Zaburi
95 Njooni tumpigie Yehova vigelegele kwa shangwe!+
Na tumpigie Mwamba wetu wa wokovu vigelegele vya ushindi.+
3 Kwa maana Yehova ni Mungu mkuu+
Na Mfalme mkuu juu ya miungu mingine yote,+
4 Yeye ambaye mkononi mwake mna vina vya ndani sana vya dunia+
Na ambaye vilele vya milima ni vyake;+
5 Ambaye bahari, aliyoiumba yeye mwenyewe, ni yake+
Na ambaye mikono yake mwenyewe iliifanyiza nchi kavu.+
6 Ingieni, tuabudu na kuinama;+
Na tupige magoti+ mbele za Yehova Mtengenezaji wetu.+
7 Kwa maana yeye ni Mungu wetu, na sisi ni watu wa malisho yake na kondoo wa mkono wake.+
Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+