Zaburi
3 Waovu wataendelea kuwako hata wakati gani, Ee Yehova,+
Waovu wataendelea kushangilia hata wakati gani?+
4 Wanaendelea kuropoka, wanaendelea kusema ovyoovyo;+
Wote wanaofanya mambo yenye kuumiza wanaendelea kujivuna wenyewe.+
8 Eleweni, ninyi msiotumia akili mlio kati ya watu;+
Nanyi wajinga, mtapata ufahamu wowote wakati gani?+
11 Yehova anazijua fikira za wanadamu, kwamba hizo ni kama pumzi.+
12 Mwenye furaha ni mwanamume ambaye unamrekebisha,+ Ee Yah,
Na ambaye unamfundisha katika sheria yako mwenyewe,+
13 Ili kumpa utulivu kutokana na siku za msiba,+
Mpaka shimo lichimbwe kwa ajili ya mwovu.+
16 Ni nani atakayesimama kwa ajili yangu juu ya waovu?+
Ni nani atakayesimama kwa ajili yangu juu ya wanaotenda mambo yenye kuumiza?+
18 Niliposema: “Hakika mguu wangu utatembea ukitikisika,”+
Fadhili zako zenye upendo, Ee Yehova, ziliendelea kunitegemeza.+
19 Fikira zangu zinazofadhaisha zilipokuwa nyingi ndani yangu,+
Faraja zako mwenyewe zilianza kuikumbatia nafsi yangu.+
20 Je, kiti cha ufalme kinachosababisha shida, kitashirikiana nawe,+
Na huku kinatunga matatizo kwa njia ya amri?+
21 Wao hushambulia vikali nafsi ya mwadilifu+
Na kutangaza kwamba damu ya mtu asiye na hatia ni yenye uovu.+
Yehova Mungu wetu atawanyamazisha.+