4 Waambieni wale wanaohangaika moyoni:+ “Iweni na nguvu.+ Msiogope.+ Tazameni! Mungu wenu atakuja na kisasi,+ Mungu akiwa na malipo.+ Yeye mwenyewe atakuja na kuwaokoa ninyi.”+
28 “Kuna sauti ya wale wanaokimbia na wale wanaoponyoka kutoka katika nchi ya Babiloni+ ili kutangaza katika Sayuni kisasi cha Yehova Mungu wetu,+ kisasi kwa ajili ya hekalu lake.+
2 Yehova ni Mungu anayetaka watu wajitoe kikamili+ na hulipiza kisasi; Yehova analipiza kisasi+ naye yuko tayari kuonyesha ghadhabu.+ Yehova anawalipiza kisasi wapinzani wake,+ naye ana kinyongo juu ya adui zake.+
6 kwamba yeyote asifikie hatua ya kudhuru na kuziingilia haki za ndugu yake katika jambo hilo,+ kwa sababu Yehova ndiye anayelipiza adhabu kwa ajili ya mambo yote haya,+ kama vile tulivyowaambia ninyi kimbele na pia tukawapa ushahidi kamili.+