Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 18
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mambo ya Walawi—Yaliyomo

      • Ngono haramu (1-30)

        • Msiwaige Wakanaani (3)

        • Ngono mbalimbali kati ya watu wa ukoo (6-18)

        • Wakati wa hedhi (19)

        • Ngono kati ya watu wa jinsia moja (22)

        • Ngono na wanyama (23)

        • ‘Msijichafue, kama sivyo, nchi itawatapika’ (24-30)

Mambo ya Walawi 18:2

Marejeo

  • +Mwa 17:7; Kut 6:7

Mambo ya Walawi 18:3

Marejeo

  • +Kut 23:24; Law 20:23

Mambo ya Walawi 18:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”

Marejeo

  • +Law 20:22; Kum 4:1

Mambo ya Walawi 18:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”

Marejeo

  • +Lu 10:27, 28; Ro 10:5; Gal 3:12

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Ufahamu,

    Mnara wa Mlinzi,

    8/15/2009, uku. 6

  • Fahirishi ya Machapisho

    w09 8/15 6

Mambo ya Walawi 18:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kufunua uchi wake.”

Marejeo

  • +Law 20:17

Mambo ya Walawi 18:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Ni uchi wa baba yako.”

Marejeo

  • +Mwa 35:22; 49:4; Law 20:11; Kum 27:20; 2Sa 16:21; 1Ko 5:1

Mambo ya Walawi 18:9

Marejeo

  • +Law 20:17; Kum 27:22; 2Sa 13:10-12

Mambo ya Walawi 18:12

Marejeo

  • +Law 20:19

Mambo ya Walawi 18:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Usifunue uchi wa.”

Marejeo

  • +Law 20:20

Mambo ya Walawi 18:15

Marejeo

  • +Law 20:12

Mambo ya Walawi 18:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ni uchi wa ndugu yako.”

Marejeo

  • +Law 20:21; Kum 25:5; Mk 6:17, 18

Mambo ya Walawi 18:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ni mwenendo wa aibu; mwenendo mchafu uliopotoka.”

Marejeo

  • +Law 20:14; Kum 27:23

Mambo ya Walawi 18:18

Marejeo

  • +Mwa 30:15

Mambo ya Walawi 18:19

Marejeo

  • +Law 15:19, 24; 20:18

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Ufahamu, uku. 372

    Mnara wa Mlinzi,

    6/1/1989, uku. 14

Mambo ya Walawi 18:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “rafiki yako.”

Marejeo

  • +Kut 20:14; Law 20:10; Kum 22:22; Met 6:29; Mt 5:27, 28; 1Ko 6:9, 10; Ebr 13:4

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Amkeni!,

    10/22/1993, uku. 30

Mambo ya Walawi 18:21

Marejeo

  • +Law 20:2; Kum 18:10; 1Fa 11:7; 2Fa 23:10
  • +Law 20:3

Mambo ya Walawi 18:22

Marejeo

  • +Mwa 19:5; Law 20:13; Amu 19:22; Ro 1:26, 27; 1Ko 6:9, 10; Yud 7

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Amkeni,

    1/2012, uku. 28

  • Fahirishi ya Machapisho

    g 1/12 28

Mambo ya Walawi 18:23

Marejeo

  • +Kut 22:19; Law 20:15, 16

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    7/15/2003, uku. 27

  • Fahirishi ya Machapisho

    w03 7/15 27

Mambo ya Walawi 18:24

Marejeo

  • +Law 20:23; Kum 18:12

Mambo ya Walawi 18:25

Marejeo

  • +Mwa 15:16

Mambo ya Walawi 18:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”

Marejeo

  • +Law 20:22; Kum 4:1, 40
  • +Kut 12:49

Mambo ya Walawi 18:27

Marejeo

  • +Kum 20:17, 18; 2Fa 16:2, 3; 21:1, 2

Mambo ya Walawi 18:30

Marejeo

  • +Law 18:3; 20:23; Kum 18:9

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

Law. 18:2Mwa 17:7; Kut 6:7
Law. 18:3Kut 23:24; Law 20:23
Law. 18:4Law 20:22; Kum 4:1
Law. 18:5Lu 10:27, 28; Ro 10:5; Gal 3:12
Law. 18:6Law 20:17
Law. 18:8Mwa 35:22; 49:4; Law 20:11; Kum 27:20; 2Sa 16:21; 1Ko 5:1
Law. 18:9Law 20:17; Kum 27:22; 2Sa 13:10-12
Law. 18:12Law 20:19
Law. 18:14Law 20:20
Law. 18:15Law 20:12
Law. 18:16Law 20:21; Kum 25:5; Mk 6:17, 18
Law. 18:17Law 20:14; Kum 27:23
Law. 18:18Mwa 30:15
Law. 18:19Law 15:19, 24; 20:18
Law. 18:20Kut 20:14; Law 20:10; Kum 22:22; Met 6:29; Mt 5:27, 28; 1Ko 6:9, 10; Ebr 13:4
Law. 18:21Law 20:2; Kum 18:10; 1Fa 11:7; 2Fa 23:10
Law. 18:21Law 20:3
Law. 18:22Mwa 19:5; Law 20:13; Amu 19:22; Ro 1:26, 27; 1Ko 6:9, 10; Yud 7
Law. 18:23Kut 22:19; Law 20:15, 16
Law. 18:24Law 20:23; Kum 18:12
Law. 18:25Mwa 15:16
Law. 18:26Law 20:22; Kum 4:1, 40
Law. 18:26Kut 12:49
Law. 18:27Kum 20:17, 18; 2Fa 16:2, 3; 21:1, 2
Law. 18:30Law 18:3; 20:23; Kum 18:9
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Mambo ya Walawi 18:1-30

Mambo ya Walawi

18 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 2 “Waambie Waisraeli hivi: ‘Mimi ni Yehova Mungu wenu.+ 3 Msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Misri ambako mliishi, wala msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Kanaani ambako nawapeleka.+ Msifuate sheria zao. 4 Mnapaswa kutekeleza sheria zangu,* nanyi mnapaswa kutii amri zangu na kuzifuata.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu. 5 Ni lazima mshike amri zangu na sheria zangu;* yeyote anayefanya hivyo ataishi kupitia hizo.+ Mimi ni Yehova.

6 “‘Hakuna mtu yeyote kati yenu anayepaswa kumkaribia mtu wake wa karibu wa ukoo ili kufanya naye ngono.*+ Mimi ni Yehova. 7 Usifanye ngono na baba yako wala mama yako. Yeye ni mama yako, usifanye naye ngono.

8 “‘Usifanye ngono na mke wa baba yako.+ Utamwaibisha baba yako.*

9 “‘Usifanye ngono na dada yako, awe ni binti ya baba yako au binti ya mama yako, awe amezaliwa katika nyumba ileile au amezaliwa nje.+

10 “‘Usifanye ngono na binti ya mwana wako au binti ya binti yako, kwa sababu ni uchi wako mwenyewe.

11 “‘Usifanye ngono na binti ya mke wa baba yako, mtoto wa baba yako, kwa sababu ni dada yako.

12 “‘Usifanye ngono na dada ya baba yako. Ana uhusiano wa damu na baba yako.+

13 “‘Usifanye ngono na dada ya mama yako, kwa sababu ana uhusiano wa damu na mama yako.

14 “‘Usimwaibishe* ndugu ya baba yako kwa kufanya ngono na mke wake. Mke huyo ni shangazi yako.+

15 “‘Usifanye ngono na binti mkwe wako.+ Yeye ni mke wa mwana wako, usifanye naye ngono.

16 “‘Usifanye ngono na mke wa ndugu yako,+ kwa sababu utamwaibisha ndugu yako.*

17 “‘Usifanye ngono na mwanamke na binti yake.+ Usimchukue binti ya mwana wa mwanamke huyo na binti ya binti yake ili kufanya nao ngono. Wao ni watu wake wa karibu wa ukoo; hilo ni tendo chafu linalochukiza.*

18 “‘Usimchukue dada ya mke wako ili awe mke mwenza+ na kufanya naye ngono wakati mke wako angali hai.

19 “‘Usimkaribie mwanamke wakati wa hedhi anapokuwa si safi ili kufanya naye ngono.+

20 “‘Usifanye ngono na mke wa jirani yako* na hivyo kujichafua.+

21 “‘Usikubali mtoto wako yeyote atolewe dhabihu kwa Moleki.+ Usilichafue jina la Mungu wako kwa njia hiyo.+ Mimi ni Yehova.

22 “‘Usilale na mwanamume kama vile unavyolala na mwanamke.+ Ni tendo linalochukiza.

23 “‘Mwanamume hapaswi kujichafua kwa kufanya ngono na mnyama; wala mwanamke hapaswi kwenda kufanya ngono na mnyama.+ Kufanya hivyo kunakiuka sheria ya asili.

24 “‘Msijichafue kwa kufanya jambo lolote kati ya mambo hayo, kwa maana mataifa ninayoyafukuza kutoka mbele yenu yamejichafua kwa mambo hayo yote.+ 25 Kwa hiyo nchi si safi, nami nitaiadhibu kwa sababu ya dhambi yake, nayo nchi itawatapika wakaaji wake.+ 26 Lakini ni lazima ninyi mzishike amri zangu na sheria zangu,*+ msifanye jambo lolote kati ya mambo hayo yenye kuchukiza, awe ni mwenyeji au mgeni anayeishi miongoni mwenu.+ 27 Kwa maana mambo hayo yote yenye kuchukiza yalifanywa na watu walioishi katika nchi hiyo kabla yenu,+ na sasa nchi si safi. 28 Msifanye mambo hayo ili nchi isiwatapike kwa sababu ya kuichafua kama itakavyoyatapika mataifa yaliyowatangulia. 29 Mtu yeyote akifanya jambo lolote kati ya mambo hayo yenye kuchukiza, wote wanaofanya mambo hayo ni lazima wauawe watoke miongoni mwa watu wao. 30 Ni lazima mtimize wajibu wenu kwangu kwa kutofuata desturi yoyote kati ya desturi zenye kuchukiza zilizofuatwa kabla yenu,+ ili msijichafue kwa desturi hizo. Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki