Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/96 uku. 2
  • Mikutano ya Utumishi kwa Desemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano ya Utumishi kwa Desemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Desemba 2
  • Juma Linaloanza Desemba 9
  • Juma Linaloanza Desemba 16
  • Juma Linaloanza Desemba 23
  • Juma Linaloanza Desemba 30
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 12/96 uku. 2

Mikutano ya Utumishi kwa Desemba

Juma Linaloanza Desemba 2

Wimbo 134

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: “Ni Nani Atakayesikiliza Ujumbe Wetu?” Maswali na majibu. Tia ndani mambo makuu kutoka Amkeni! la Machi 22, 1987, ukurasa wa 5 (la Kiingereza), kuhusu sababu ujumbe wetu ni wenye kuvutia.

Dak. 20: “Neno la Mungu Huandaa Mwongozo.” (Mafungu 1-6) Toa utangulizi wa sehemu hiyo kwa mafungu 1-2. (Tia ndani kitabu Kutoa Sababu, kurasa 40-42, ukionyesha kifupi “Sababu za kutufanya tuichunguze Biblia.”) Panga watangazaji hodari watoe wonyesho wa utoaji mbalimbali katika mafungu 3-6. Alika wasikilizaji watoe maelezo juu ya (1) jinsi maswali yaliyoulizwa yalivyosaidia kuamsha kupendezwa, (2) jinsi maandiko yaliyotumiwa yanavyofaa somo lililozungumzwa, (3) jinsi ziara ya kurudia ilivyofuatia kwa kutazamiwa mazungumzo ya kwanza, na (4) jinsi toleo la funzo lilivyofanywa.

Wimbo 75 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 9

Wimbo 100

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: Kusaidia Wazee-Wazee Washiriki Katika Utumishi. Watangazaji wengi waaminifu walio wazee hutamani sana kushiriki katika mahubiri ya kutaniko, lakini hawana uwezo wa kimwili kwa sababu ya uzee na afya mbaya. Kuna njia tunazoweza kuwaonyesha ufikirio ili kuwatia ndani katika kikundi cha utumishi: Jitolee kuandaa usafiri; wapangie kuhubiri nyumba ambazo hazina ngazi nyingi za kupanda; egesha gari karibu ili waweze kupumzika wanapochoka; jitolee kuwapeleka kwenye ziara zao za kurudia; wajulishe kwamba utawapeleka nyumbani wanapohisi hawawezi kuendelea. Wazee-wazee hushukuru msaada wanaopewa. Taja njia nyinginezo mnazoonyesha ufikirio kama huo kwenu. Pitia mambo makuu yaliyoko katika makala “Twawathamini Walio Wazee!” ipatikanayo katika Mnara wa Mlinzi, Februari, 1986, kurasa 28-29, (la Kiingereza).

Dak. 20: “Neno la Mungu Huandaa Mwongozo.” (Mafungu 7-9) Toa maelezo juu ya “Uhitaji wa Mwongozo” katika Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 1993, ukurasa wa 3. Eleza sababu utoaji wetu mbalimbali wapaswa kukazia umaana wa kutafuta msaada kutoka chanzo cha juu zaidi—Mungu. Panga mtangazaji atoe wonyesho wa utoaji mbalimbali katika mafungu 7-8. Kazia kwamba mradi wetu wapaswa kuwa hatimaye kuanzisha funzo la Biblia katika kitabu Ujuzi.

Wimbo 197 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 16

Wimbo 209

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Toa madokezo kadhaa ya jinsi ya kuitikia salamu za sikukuu kwa busara. Eleza mipango ya pekee ya utumishi wa shambani ya Desemba 25.

Dak. 15: “Kujitoa kwa Hiari.” Maswali na majibu. Tia ndani maelezo kutoka Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 1984, ukurasa wa 22.

Dak. 20: “Kushangilia Ongezeko Ambalo Mungu Hutoa.” Hotuba yenye idili itolewe na mzee. Taja mambo yaliyoonwa au uthibitisho wa ongezeko katika nchi zinazowakilishwa, kama ilivyotolewa katika Vitabu-Mwaka vya karibuni.

Wimbo 41 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 23

Wimbo 93

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Onyesha mambo ya kuzungumzia katika magazeti ya karibuni yanayoweza kutumiwa katika utumishi juma hili. Eleza mipango ya pekee ya utumishi wa shambani ya Januari 1.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Au mzee atoe hotuba juu ya “Ustaafu—Mlango Ulio Wazi Kuelekea Utendaji wa Kitheokrasi?” kutoka Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1996, kurasa 24-25.—Ona Insight, Buku la 2, ukurasa 794, mafungu 2-3.

Dak. 20: “Uandikishwaji Katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Toa takwimu za walioandikishwa za kwenu, na utie moyo wote wanaoweza wajiandikishe. Pitia maagizo yaliyoko katika “Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1997.”

Wimbo 166 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 30

Wimbo 223

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ikiwa kutaniko lenu lakaribia kubadili saa za mikutano kwa mwaka mpya, toa kitia moyo chenye fadhili ukisihi wote wadumishe hudhurio la kawaida na kutaniko kwa nyakati zalo mpya.

Dak. 20: “Kusonga Mbele Kwako na Kuwe Dhahiri kwa Watu Wote.” Maswali na majibu.

Dak. 15: Pitia Toleo la Fasihi la Januari. Toa kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kabla ya 1984. Ikiwa hakuna chochote akibani, tumia kitabu Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya. Onyesha ni vitabu vipi ambavyo kutaniko linavyo akibani. Chagua viwili au vitatu ambavyo vitafaa kutumiwa katika eneo lenu. Ukitumia kitabu Kutoa Sababu, kurasa 9-14, pitia kifupi utangulizi mbalimbali unaofaa kwa kila kitabu. Toa wonyesho wa utoaji mmoja au mbili.

Wimbo 137 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki