Ayubu
3 Ilikuwa baada ya hayo kwamba Ayubu akafungua kinywa chake, akaanza kuilaani siku yake.+ 2 Basi Ayubu akajibu, akasema:
3 “Na iangamie ile siku niliyozaliwa,+
Pia ule usiku ambao mtu alisema, ‘Mwanamume amechukuliwa mimba!’
5 Giza na kivuli kizito kiichukue.
Wingu la mvua na likae juu yake.
Vitu vinavyotia mchana giza na viitie hofu.+
6 Usiku huo—giza na liuchukue;+
Usiwe na furaha katikati ya siku za mwaka;
Usiingie katikati ya hesabu ya miezi.
9 Nyota za wakati wa gizagiza lake na ziingiwe na giza;
Na ungojee nuru wala kusiwe na yoyote;
Nao usiione miali ya mapambazuko.
10 Kwa maana haukufunga milango ya tumbo la uzazi la mama yangu,+
Na hivyo kuficha taabu kutoka machoni pangu.
13 Kwa maana kufikia sasa ningalikuwa nimelala ili nisisumbuliwe;+
Ningalilala wakati huo; ningalikuwa ninapumzika+
14 Pamoja na wafalme na washauri wa dunia,+
Wale wanaojijengea mahali penye ukiwa,+
15 Au pamoja na wakuu walio na dhahabu,
Wale wanaozijaza nyumba zao fedha;
16 Au, kama mimba yenye kuharibika+ iliyofichwa, singalikuwako,
Kama watoto ambao hawajaona nuru.+
21 Kwa nini kuna wale wanaongojea kifo, wala hakipo,+
Ijapokuwa wanaendelea kuchimba wakikitafuta kuliko kutafuta hazina zilizofichwa?
22 Wale wanaoshangilia kwa raha,
Wanafurahi kwa sababu wanapata kaburi.
23 Kwa nini anampa nuru mwanamume, ambaye njia yake imefichwa,+
Na ambaye Mungu anamzungushia ukuta?+
24 Kwa maana kuugua kwangu huja mbele ya chakula changu,+
Na vilio vyangu vya kunguruma+ humwagika kama maji;
25 Kwa sababu nimehofu kitu chenye kutia hofu, nacho kinakuja juu yangu;
Na kile ambacho nimekiogopa kinanijia.+
26 Mimi sijawa bila mahangaiko, wala sijawa bila usumbufu,
Wala sijawa na pumziko, na bado msukosuko unakuja.”