Hesabu
10 Na Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 2 “Jifanyie tarumbeta+ mbili za fedha. Utazifua, nawe utazitumia kuliita+ kusanyiko na kwa ajili ya kuzivunja kambi. 3 Nao watazipiga zote mbili, nalo kusanyiko lote litakutana nawe kwenye mwingilio wa hema la mkutano.+ 4 Na ikiwa watapiga moja tu, ndipo wakuu wakiwa vichwa vya maelfu ya Israeli watakutana nawe kama ilivyopangwa.+
5 “Nanyi mtapiga mvumo unaopanda na kushuka, nazo kambi za wale wanaopiga kambi upande wa mashariki+ zitaondoka. 6 Nanyi mtapiga mvumo unaopanda na kushuka kwa mara ya pili, nazo kambi za wale wanaopiga kambi upande wa kusini+ zitaondoka. Watapiga mvumo unaopanda na kushuka kila mara moja kati yazo inapoondoka.
7 “Sasa wakati wa kuita kutaniko pamoja, mtapiga,+ lakini hamtapiga mvumo unaopanda na kushuka. 8 Nao wana wa Haruni, kuhani, watazipiga tarumbeta,+ nazo zitakuwa sheria kwa ajili yenu mpaka wakati usio na kipimo katika vizazi vyenu.
9 “Na ikiwa mtaingia vitani katika nchi yenu kupigana na mkandamizaji anayewasumbua ninyi,+ mnapaswa pia kutoa mwito wa vita kwa tarumbeta+ nanyi hakika mtakumbukwa mbele za Yehova Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.+
10 “Na katika siku ya kushangilia+ kwenu na katika majira yenu ya sherehe+ na mwanzoni mwa miezi yenu,+ mtapiga tarumbeta juu ya matoleo yenu ya kuteketezwa+ na dhabihu zenu za ushirika;+ nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Yehova Mungu wenu. Mimi ni Yehova Mungu wenu.”+
11 Sasa ikawa kwamba katika mwaka wa pili, katika mwezi wa pili, siku ya 20 katika mwezi huo,+ lile wingu likainuka kutoka juu ya maskani+ ya Ushuhuda. 12 Nao wana wa Israeli wakaanza kuondoka katika namna ya kuondoka+ kwao kutoka katika nyika ya Sinai, nalo wingu likakaa katika nyika ya Parani.+ 13 Nao wakaanza kuondoka kwa mara ya kwanza, kulingana na agizo la Yehova kupitia Musa.+
14 Kwa hiyo ule mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya wana wa Yuda ndio ulioondoka kwanza kabisa, kwa majeshi yao,+ naye Nashoni+ mwana wa Aminadabu alikuwa juu ya jeshi la mgawanyo huo. 15 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Isakari kulikuwa na Nethaneli+ mwana wa Zuari. 16 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Zabuloni kulikuwa na Eliabu mwana wa Heloni.+
17 Nayo maskani ikashushwa,+ nao wana wa Gershoni+ na wana wa Merari,+ wakiwa wachukuzi wa maskani wakaondoka.
18 Nao ule mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya Rubeni+ ukaondoka, kwa majeshi yao, naye Elisuri+ mwana wa Shedeuri alikuwa juu ya jeshi lake. 19 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Simeoni+ kulikuwa na Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 20 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Gadi kulikuwa na Eliasafu+ mwana wa Deueli.
21 Nao Wakohathi wakiwa wachukuzi wa patakatifu+ wakaondoka, kwa maana watakuwa wameisimamisha maskani kufikia wakati wa kuja kwao.
22 Na ule mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya wana wa Efraimu+ ukaondoka, kwa majeshi yao, naye Elishama+ mwana wa Amihudi alikuwa juu ya jeshi lake. 23 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Manase+ kulikuwa na Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 24 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Benyamini+ kulikuwa na Abidani+ mwana wa Gidioni.
25 Na ule mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya wana wa Dani+ ukaondoka ukifanyiza kikosi cha nyuma cha ulinzi+ kwa ajili ya kambi zote, kwa majeshi yao, naye Ahiezeri+ mwana wa Amishadai alikuwa juu ya jeshi lake. 26 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Asheri+ kulikuwa na Pagieli+ mwana wa Okrani. 27 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Naftali+ kulikuwa na Ahira+ mwana wa Enani. 28 Hivyo ndivyo wana wa Israeli walivyoondoka, kwa majeshi yao, walipokuwa wakiondoka.+
29 Ndipo Musa akamwambia Hobabu mwana wa Reueli+ Mmidiani, baba-mkwe wa Musa: “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Yehova alisema, ‘Nitawapa ninyi.’+ Nenda pamoja nasi, nasi hakika tutakutendea mema,+ kwa sababu Yehova amesema mema juu ya Israeli.”+ 30 Lakini akamwambia: “Sitaenda pamoja nanyi, bali nitaenda katika nchi yangu+ mwenyewe na kwa jamaa zangu.” 31 Basi akasema: “Tafadhali, usituache, kwa sababu unajua vema mahali ambapo tunaweza kupiga kambi nyikani, utakuwa macho yetu. 32 Na itakuwa kwamba ikiwa utaenda pamoja nasi,+ naam, itakuwa kwamba wema ambao Yehova atatutendea, sisi nasi tutakutendea wewe.”
33 Kwa hiyo wakapiga mwendo kutoka mlima wa Yehova+ safari ya siku tatu, nalo sanduku la agano+ la Yehova lilikuwa likipiga mwendo mbele yao kwa safari ya siku tatu ili kutafuta mahali pa kupumzika kwa ajili yao.+ 34 Nalo wingu+ la Yehova lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipokuwa wakipiga mwendo kutoka katika kambi.
35 Na ikawa kwamba Sanduku lilipokuwa likiondoka, Musa alikuwa akisema: “Usimame, Ee Yehova, adui zako na watawanyike;+ na wale wanaokuchukia vikali wakimbie toka mbele zako.”+ 36 Na lilipopumzika, alikuwa akisema: “Urudi, Ee Yehova, kwa makumi ya maelfu ya maelfu ya Israeli.”+