Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 32:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Wao wamenichochea niwe na wivu kwa kile ambacho si mungu;+

      Wameniudhi kwa sanamu zao za ubatili;+

      Na mimi, nitawachochea wawe na wivu kwa kile ambacho si kikundi cha watu;+

      Kwa taifa jinga nitawatia uchungu.+

  • 1 Samweli 12:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Nanyi msigeuke kando ili kufuata vitu visivyo vya kweli+ ambavyo havina faida+ yoyote na ambavyo havikomboi, kwa sababu hivyo ni vitu visivyo vya kweli.

  • 2 Wafalme 17:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 nao wakaendelea kukataa masharti yake na agano+ lake alilofanya na mababu zao na vikumbusho+ vyake alivyokuwa amewaonya navyo, nao wakaendelea kufuata sanamu za ubatili+ nao wenyewe wakawa ubatili,+ naam, kwa kuiga mataifa yaliyowazunguka pande zote, ambao Yehova alikuwa amewaamuru wasifanye kama wao;+

  • Isaya 41:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Tazama! Wote ni kitu ambacho hakipo. Kazi zao si kitu. Sanamu zao za kuyeyushwa ni upepo na ubatili.+

  • Yeremia 10:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kila mtu amejiendesha kwa kukosa sana kutumia akili asiweze kujua.+ Hakika kila fundi wa chuma ataona aibu kwa sababu ya sanamu ya kuchongwa;+ kwa maana sanamu yake ya kuyeyushwa ni uwongo,+ na hamna roho ndani yake.+

  • Matendo 14:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 na kusema: “Wanaume, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi pia ni wanadamu+ tulio na udhaifu+ uleule kama ninyi, nasi tunawatangazia ninyi habari njema, ili mgeuke kutoka kwa mambo haya ya bure+ mpate kumjia Mungu aliye hai,+ aliyefanya mbingu+ na dunia na bahari na vitu vyote vilivyomo.

  • Waroma 1:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 na kuugeuza utukufu+ wa Mungu asiye na uharibifu kuwa kitu kama sanamu+ ya mwanadamu aliye na uharibifu na ya ndege na viumbe vyenye miguu minne na vitu vinavyotambaa.+

  • 1 Wakorintho 8:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Sasa kuhusu kula+ vyakula vinavyotolewa kwa sanamu, tunajua kwamba sanamu si kitu+ katika ulimwengu, na kwamba hakuna Mungu isipokuwa mmoja.+

  • 1 Wakorintho 10:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Basi, niseme nini? Kwamba kile ambacho kimetolewa dhabihu kwa sanamu ni kitu, au kwamba sanamu ni kitu?+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki