Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 36:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki+ wale wajumbe wa Mungu wa kweli na kuyadharau maneno+ yake na kuwafanyia mzaha+ manabii wake, mpaka ghadhabu+ ya Yehova ikapanda juu ya watu wake, mpaka kukawa hakuna kuponywa.+

  • Nehemia 9:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “Hata hivyo, wakakosa kutii,+ wakakuasi+ na kuzidi kutupa sheria yako nyuma ya migongo yao,+ wakawaua manabii wako mwenyewe,+ waliotoa ushahidi juu yao ili kuwarudisha kwako;+ nao wakaendelea kutenda matendo ya ukosefu mkubwa wa heshima.+

  • Mathayo 21:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Hata hivyo, wakulima wakawachukua watumwa wake, wakampiga mmoja sana, mwingine wakamuua, mwingine wakampiga kwa mawe.+

  • Mathayo 23:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Kwa sababu hiyo, tazameni, ninatuma+ kwenu manabii na watu wenye hekima na wafundishaji wa watu wote.+ Baadhi yao mtawaua+ na kuwatundika mtini, na baadhi yao mtawapiga mijeledi+ katika masinagogi yenu na kuwatesa jiji baada ya jiji;

  • Matendo 7:52
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 52 Ni yupi kati ya manabii ambaye mababu zenu hawakumtesa?+ Ndiyo, waliwaua+ wale waliotangaza kimbele kuhusu kuja kwa Aliye mwadilifu,+ ambaye ninyi sasa mmemsaliti na kumuua,+

  • 1 Wathesalonike 2:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 waliomuua hata Bwana Yesu+ na manabii+ na kututesa sisi.+ Zaidi ya hayo, wao hawampendezi Mungu, bali wako kinyume cha faida za wanadamu wote,

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki