Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 17:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 na Yehova akaendelea kuonya+ Israeli+ na Yuda+ kupitia manabii+ wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni kutoka katika njia zenu mbaya,+ mshike amri+ zangu, sheria+ zangu, kulingana na sheria+ yote niliyowaamuru mababu+ zenu na ambayo nimepeleka kwenu kupitia watumishi wangu manabii”;+

  • Isaya 55:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Mtu mwovu aiache njia yake,+ na mtu mwenye madhara ayaache mawazo yake;+ naye arudi kwa Yehova, ambaye atamwonyesha rehema,+ na kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.+

  • Yeremia 18:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “Na sasa, tafadhali, waambie watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, ‘Yehova amesema hivi: “Tazama, ninafanya msiba juu yenu na kutafakari wazo fulani juu yenu.+ Geukeni, tafadhali, kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya, na mfanye njia zenu na matendo yenu kuwa mema.”’”+

  • Yeremia 35:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Nami niliendelea kutuma kwenu watumishi wangu wote manabii,+ nikiamka mapema na kuwatuma, na kusema, ‘Tafadhali rudini, kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya,+ nanyi fanyeni matendo yenu kuwa mema,+ wala msiifuate miungu mingine ili kuitumikia.+ Na mwendelee kukaa katika nchi ambayo nimewapa ninyi na mababu zenu.’+ Lakini hamkutega sikio lenu, wala hamkunisikiliza.+

  • Ezekieli 18:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 “ ‘Kwa hiyo nitawahukumu ninyi kila mmoja kulingana na njia yake,+ Ee nyumba ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+ ‘Geukeni, naam, geukeni na kuyaacha makosa yenu yote,+ na chochote kisiwe kwenu kikwazo kinachosababisha kosa.+

  • Ezekieli 33:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Waambie, ‘ “Kama ninavyoishi,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, “Ninapendezwa, si na kifo cha mwovu,+ bali kwamba mtu mwovu ageuke na kuiacha+ njia yake na kwa kweli aendelee kuishi.+ Geukeni, geukeni mziache njia zenu mbaya,+ maana kwa nini mfe, Ee nyumba ya Israeli?” ’+

  • Yona 3:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Nao wajifunike nguo za magunia, mwanadamu na mnyama wa kufugwa; na wamwite Mungu kwa nguvu na warudi,+ kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya na kutoka katika jeuri iliyokuwa mikononi mwao.

  • Zekaria 1:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 “ ‘Msiwe kama baba zenu+ ambao manabii wa kale waliwaita,+ wakisema: “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Tafadhali, rudini mwache njia zenu mbaya na mwache matendo yenu mabaya.’ ” ’+

      “ ‘Lakini hawakusikiliza, wala hawakunitegea sikio,’+ asema Yehova.

  • Malaki 3:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Tangu siku za mababu zenu mmeyaacha masharti yangu wala hamkuyashika.+ Rudini kwangu, nami nitarudi kwenu,”+ Yehova wa majeshi amesema.

      Nanyi mmesema: “Tutarudi kwa njia gani?”

  • 2 Petro 3:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Yehova hakawii kuhusiana na ahadi yake,+ kama watu fulani wanavyoona kukawia, bali yeye ni mwenye subira kwenu kwa sababu hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki