11 Mtu yeyote wa Yeroboamu atakayekufa jijini, mbwa watamla;+ na yule atakayekufa shambani, ndege wa angani watamla,+ kwa sababu Yehova mwenyewe amesema hayo.”’
4 ‘Watakufa vifo vya magonjwa.+ Hawataombolezewa,+ wala hawatazikwa.+ Watakuwa kama mbolea juu ya uso wa nchi;+ nao watamalizwa kwa upanga na kwa njaa,+ na maiti zao kwa kweli zitakuwa chakula kwa viumbe vinavyoruka vya mbinguni na kwa wanyama wa duniani.’+
7 Nami nitalivunja shauri la Yuda na la Yerusalemu mahali hapa,+ nami nitawaangusha kwa upanga mbele ya adui zao na kwa mkono wa wale wanaoitafuta nafsi yao.+ Na maiti zao nitazitoa ziwe chakula kwa viumbe vinavyoruka vya mbinguni na kwa wanyama wa dunia.+