-
2 Wafalme 23:5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Naye akawaondoa kazini makuhani wa miungu ya kigeni, ambao wafalme wa Yuda walikuwa wameweka ili wapate kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu katika majiji ya Yuda na ujirani wa Yerusalemu, na pia wale wanaofukiza moshi wa dhabihu kwa Baali,+ kwa jua na kwa mwezi na kwa makundi-nyota ya unajimu na kwa jeshi lote la mbinguni.+
-
-
Ezekieli 8:16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Kwa hiyo akanileta katika ua wa ndani wa nyumba ya Yehova,+ na, tazama! kwenye mwingilio wa hekalu la Yehova, katikati ya ukumbi na madhabahu,+ kulikuwa na wanaume 25+ hivi migongo yao ikielekea hekalu la Yehova+ na nyuso zao zikielekea mashariki, nao walikuwa wameelekea mashariki, wakiliinamia jua.+
-