Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 4:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 wala usije ukayainua macho yako mbinguni na kuona jua na mwezi na nyota, jeshi lote la mbinguni, nawe upate kushawishiwa na kuviinamia na kuvitumikia,+ vile ambavyo Yehova Mungu wako amegawia vikundi vyote vya watu chini ya mbingu nzima.+

  • Kumbukumbu la Torati 17:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 naye aende na kuabudu miungu mingine na kuinamia hiyo au jua au mwezi au jeshi lote la mbinguni,+ jambo ambalo sijaamuru,+

  • 2 Wafalme 17:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Nao wakaendelea kuacha amri+ zote za Yehova, Mungu wao, wakajitengenezea sanamu za kuyeyushwa,+ ndama wawili,+ na kutengeneza mti mtakatifu,+ nao wakaanza kuliinamia jeshi lote la mbinguni+ na kutumikia Baali;+

  • 2 Wafalme 23:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Naye akawaondoa kazini makuhani wa miungu ya kigeni, ambao wafalme wa Yuda walikuwa wameweka ili wapate kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu katika majiji ya Yuda na ujirani wa Yerusalemu, na pia wale wanaofukiza moshi wa dhabihu kwa Baali,+ kwa jua na kwa mwezi na kwa makundi-nyota ya unajimu na kwa jeshi lote la mbinguni.+

  • Ayubu 31:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Ikiwa nilikuwa nikiona nuru wakati ilipowaka,

      Au mwezi wenye fahari ukisonga,+

  • Yeremia 8:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Nao kwa kweli wataitandaza mbele ya jua na mbele ya mwezi na mbele ya jeshi lote la mbingu ambalo wamelipenda na ambalo wamelitumikia na ambalo wamelifuata+ na ambalo wamelitafuta na ambalo wameliinamia.+ Haitakusanywa, wala haitazikwa. Itakuwa kama mbolea juu ya uso wa nchi.”+

  • Yeremia 44:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 lakini hakika tutafanya kila neno ambalo limetoka katika kinywa chetu,+ ili kumfukizia ‘malkia wa mbingu’+ moshi wa dhabihu na kummiminia matoleo ya kinywaji,+ kama sisi wenyewe+ na mababu+ zetu, wafalme+ wetu na wakuu wetu tulivyofanya katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu, wakati tuliposhiba mkate na kuwa na hali njema, nasi hatukuona msiba wowote kamwe.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki