Ayubu
42 Naye Ayubu akamjibu Yehova, akasema:
2 “Nimepata kujua kwamba unaweza kufanya mambo yote,+
Wala hakuna wazo lolote ambalo huwezi kulifikia.+
3 ‘Ni nani huyu anayefunika shauri bila ujuzi?’+
Kwa hiyo nilisema, lakini sikuwa ninaelewa
Mambo yaliyo ya ajabu mno kwangu, ambayo siyajui.+
5 Nimesikia habari zako kwa fununu,
Lakini sasa jicho langu mwenyewe linakuona wewe.
7 Na ikawa baada ya Yehova kumwambia Ayubu maneno hayo, ndipo Yehova akamwambia Elifazi Mtemani:
“Hasira yangu imewaka juu yako na rafiki zako wawili,+ kwa maana ninyi hamkusema mambo ya kweli+ kunihusu mimi kama mtumishi wangu Ayubu. 8 Na sasa chukueni ng’ombe-dume saba+ na kondoo-dume saba+ kisha mwende kwa mtumishi wangu Ayubu, nanyi mtoe dhabihu ya kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe; na Ayubu mtumishi wangu atasali kwa ajili yenu.+ Nitakubali uso wake peke yake ili nisiwatendee ninyi upumbavu wenye kufedhehesha, kwa maana hamkusema mambo ya kweli kunihusu mimi, kama mtumishi wangu Ayubu.”+
9 Basi Elifazi Mtemani na Bildadi Mshua na Sofari Mnaamathi wakaenda, wakafanya kama Yehova alivyowaambia; na kwa hiyo Yehova akaukubali uso wa Ayubu.
10 Na Yehova akaigeuza hali ya mateka ya Ayubu+ aliposali kwa ajili ya wale rafiki zake,+ na Yehova akaanza kumpa na kumwongezea Ayubu vyote vilivyokuwa vyake, kiasi cha mara mbili.+ 11 Na ndugu zake wote na dada zake wote na wale wote waliokuwa wakimjua+ hapo mwanzoni wakaendelea kuja kwake, nao wakaanza kula mkate pamoja naye+ katika nyumba yake na kusikitika pamoja naye na kumfariji juu ya msiba wote ambao Yehova alikuwa ameuruhusu uje juu yake; nao wakaanza kila mmoja wao kumpa kipande cha pesa na kila mmoja pete ya dhahabu.
12 Naye Yehova akaubariki+ mwisho wa Ayubu baadaye kuliko mwanzo wake,+ hivi kwamba akawa na kondoo kumi na nne elfu na ngamia elfu sita na jozi elfu moja za ng’ombe na punda-jike elfu moja. 13 Pia akawa na wana saba na binti watatu.+ 14 Naye akamwita yule wa kwanza jina Yemima na yule wa pili Kezia na yule wa tatu Kereni-hapuku. 15 Na hapakuonekana wanawake wowote walio warembo kama wale binti za Ayubu katika nchi yote, na baba yao akawapa urithi katikati ya ndugu zao.+
16 Naye Ayubu akaendelea kuishi miaka 140+ baada ya mambo hayo, akaona wanawe na wajukuu wake+—vizazi vinne. 17 Na mwishowe Ayubu akafa, akiwa mzee na mwenye kushiba siku.+