Waebrania
Kwa Waebrania
1 Mungu, ambaye zamani za kale alisema katika pindi nyingi+ na katika njia nyingi na mababu zetu kupitia manabii,+ 2 mwishoni mwa siku hizi+ amesema nasi kupitia Mwana,+ aliyemweka rasmi kuwa mrithi wa vitu vyote,+ na ambaye kupitia yeye aliifanya+ mifumo ya mambo. 3 Yeye ndiye mng’ao wa utukufu+ wake na mwakilisho sawasawa wa utu wake wenyewe,+ naye hutegemeza vitu vyote kwa neno la nguvu zake;+ na akiisha kuzitakasa dhambi+ zetu aliketi kwenye mkono wa kuume+ wa Ukuu katika mahali pa juu sana.+ 4 Kwa hiyo amekuwa bora kuliko malaika,+ kwa kuwa amerithi jina+ bora kabisa kuliko lao.
5 Kwa mfano, alipata kumwambia nani kati ya malaika: “Wewe ni mwanangu; mimi, leo, nimekuwa baba yako”?+ Na tena: “Mimi mwenyewe nitakuwa baba yake, na yeye mwenyewe atakuwa mwanangu”?+ 6 Lakini anapomleta tena Mzaliwa wake wa kwanza+ katika dunia inayokaliwa, yeye asema: “Malaika+ wote wa Mungu na wamsujudie.”+
7 Pia, kuwahusu malaika yeye anasema: “Naye anawafanya malaika zake kuwa roho, na watumishi wake wa watu wote kuwa mwali wa moto.”+ 8 Lakini kumhusu Mwana: “Mungu ni kiti chako cha ufalme milele+ na milele, na fimbo ya enzi ya ufalme+ wako ni fimbo ya unyoofu.+ 9 Uliupenda uadilifu, nawe ukauchukia uasi-sheria. Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, alikutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia kuliko wenzako.”+ 10 Na: “Wewe pale mwanzoni, Ee Bwana, uliiweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi za mikono yako.+ 11 Hizo zitaangamia, lakini wewe mwenyewe utabaki sikuzote; nazo zote zitachakaa kama vazi la nje,+ 12 nawe utazikunja kama kanzu,+ kama vazi la nje; nazo zitabadilishwa, lakini wewe ni yuleyule, nayo miaka yako haitakwisha kamwe.”+
13 Lakini amepata kusema hivi kuhusu nani kati ya malaika: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume, mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako”?+ 14 Je, wao wote si roho+ kwa ajili ya utumishi wa watu wote,+ waliotumwa kuhudumu kwa ajili ya wale watakaorithi+ wokovu?