Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Wimbo.
2 Ee msikiaji wa sala, kwako wewe watu wote wenye mwili watakuja.+
4 Mwenye furaha ni yule unayemchagua na kumfanya akaribie,+
Ili apate kukaa katika nyua zako.+
Hakika tutashiba mema ya nyumba yako,+
Mahali patakatifu pa hekalu lako.+
5 Utatujibu kwa mambo yenye kuogopesha katika uadilifu,+
Ee Mungu wa wokovu wetu,+
Tegemeo la mipaka yote ya dunia na wale walio mbali baharini.+
8 Na wakaaji wa sehemu za mbali zaidi wataogopa ishara zako;+
Unafanya kutokea kwa asubuhi na jioni kupige vigelegele kwa shangwe.+
9 Umeielekezea dunia fikira zako, ili uipatie wingi;+
Unaitajirisha sana.
Kijito kinachotoka kwa Mungu kimejaa maji.+
Wewe unatayarisha nafaka yao,+
Kwa maana hivyo ndivyo unavyoitayarisha dunia.+
10 Mitaro yake inajazwa maji, madonge yake yanasawazishwa;+
Unailainisha kwa manyunyu mengi; unaibariki mimea yake.+