Zekaria
3 Naye akanionyesha Yoshua+ kuhani mkuu akiwa amesimama mbele ya malaika wa Yehova, naye Shetani+ akiwa amesimama kwenye mkono wake wa kuume ili kumpinga.+ 2 Kisha malaika+ wa Yehova akamwambia Shetani: “Yehova akukemee,+ Ee Shetani, ndiyo, Yehova akukemee, yeye ambaye analichagua Yerusalemu!+ Je, huyu si kipande cha mti kilichonyakuliwa kutoka motoni?”+
3 Yoshua naye alikuwa amevaa mavazi machafu+ akiwa amesimama mbele ya malaika. 4 Ndipo akajibu na kuwaambia wale waliosimama mbele yake: “Mvueni mavazi hayo machafu.” Naye akaendelea kumwambia: “Ona, nimekuondolea kosa lako,+ nawe umevikwa kanzu za fahari.”+
5 Basi nikasema: “Na wamvike kilemba safi kichwani pake.”+ Nao wakaweka kilemba hicho safi kichwani pake na kumvika mavazi; naye malaika wa Yehova alikuwa amesimama karibu. 6 Ndipo malaika wa Yehova akaanza kumtolea Yoshua ushahidi, akisema: 7 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Ukitembea katika njia zangu, nawe ukishika wajibu wangu,+ basi wewe ndiye utakayeihukumu nyumba yangu+ na kuzitunza nyua zangu pia; nami nitakupa uhuru wa kuingia katikati ya hawa wanaosimama karibu.’
8 “ ‘Tafadhali sikia, Ee Yoshua kuhani mkuu, wewe pamoja na wenzako wanaoketi mbele yako, kwa maana wao ni watu wanaotumika kuwa ishara;+ kwa maana, tazama, mimi namleta ndani Chipukizi+ mtumishi wangu!+ 9 Kwa maana tazama! jiwe+ ambalo nimeweka mbele ya Yoshua! Juu ya jiwe hilo moja kuna macho saba.+ Tazama, mimi ninachora mchoro wake,’+ asema Yehova wa majeshi, ‘nami nitaondolea mbali kosa la nchi hiyo katika siku moja.’+
10 “ ‘Katika siku hiyo,’ asema Yehova wa majeshi, ‘Mtaitana mtu na mwenzake, mkiwa chini ya mzabibu na mkiwa chini ya mtini.’ ”+