Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+
48 Yehova ni mkuu na wa kusifiwa sana+
Katika jiji la Mungu wetu,+ katika mlima wake mtakatifu.+
2 Wenye ukuu wa kupendeza, shangwe ya dunia yote,+
Ni Mlima Sayuni ulioko sehemu za mbali za kaskazini,+
Mji wa Mfalme Mkuu.+
3 Katika minara ya makao yake Mungu amejulikana kuwa kilele salama.+
4 Kwa maana, Tazama! wafalme wenyewe wamekutana kwa mapatano,+
Wamepita karibu wakiwa pamoja.+
5 Wao wenyewe waliona; nao wakashangaa.
Wakasumbuka, wakakimbizwa wakiwa na wasiwasi mkubwa.+
6 Wakashikwa na kutetemeka wakiwa huko,+
Uchungu wa kuzaa kama ule wa mwanamke anayezaa.+
7 Kwa upepo wa mashariki wewe unavunja meli za Tarshishi.+
8 Kama vile tulivyosikia, ndivyo tumeona+
Katika jiji la Yehova wa majeshi, katika jiji la Mungu wetu.+
Mungu mwenyewe atalifanya imara mpaka wakati usio na kipimo.+ Sela
9 Tumefikiria kwa uzito, Ee Mungu, juu ya fadhili zako zenye upendo+
Katikati ya hekalu lako.+
10 Kama jina lako,+ Ee Mungu, ndivyo ilivyo sifa yako
Mpaka kwenye miisho ya dunia.
Mkono wako wa kuume umejaa uadilifu.+
11 Mlima Sayuni+ na ushangilie,
Miji ya kandokando ya Yuda na ishangilie,+ kwa sababu ya maamuzi yako ya hukumu.+
12 Pigeni mwendo mkizunguka Sayuni, na kuuzunguka-zunguka;+
Hesabuni minara yake.+
13 Wekeni mioyo yenu juu ya boma lake.+
Kagueni minara ya makao yake,
Ili mpate kukisimulia kizazi cha wakati ujao.+
14 Kwa maana Mungu huyu ni Mungu wetu mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
Yeye mwenyewe atatuongoza mpaka tufe.+