Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 31
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Kumbukumbu la Torati—Yaliyomo

      • Musa akaribia kufa (1-8)

      • Sheria yasomwa hadharani (9-13)

      • Yoshua awekwa kuwa kiongozi (14, 15)

      • Uasi wa Waisraeli watabiriwa (16-30)

        • Wimbo wa kuwafundisha Waisraeli (19, 22, 30)

Kumbukumbu la Torati 31:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kutoka nje na kuingia ndani.”

Marejeo

  • +Kut 7:7; Kum 34:7; Mdo 7:23
  • +Hes 20:12; Kum 3:27

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    10/1/2006, uku. 31

  • Fahirishi ya Machapisho

    w06 10/1 31

Kumbukumbu la Torati 31:3

Marejeo

  • +Kum 9:3
  • +Hes 27:18; Kum 3:28; Yos 1:2

Kumbukumbu la Torati 31:4

Marejeo

  • +Hes 21:23, 24
  • +Hes 21:33, 35
  • +Kut 23:23

Kumbukumbu la Torati 31:5

Marejeo

  • +Hes 33:52; Kum 7:2, 24; 20:16

Kumbukumbu la Torati 31:6

Marejeo

  • +Yos 1:6; Zb 27:14; 118:6
  • +Hes 14:9; Kum 7:18
  • +Kum 4:31; Yos 1:5; Ebr 13:5

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    8/15/1998, kur. 10-11

  • Fahirishi ya Machapisho

    w98 8/15 10-11

Kumbukumbu la Torati 31:7

Marejeo

  • +Yos 10:25
  • +Kum 1:38

Kumbukumbu la Torati 31:8

Marejeo

  • +Kut 33:14
  • +Yos 1:9

Kumbukumbu la Torati 31:9

Marejeo

  • +Kut 34:27

Kumbukumbu la Torati 31:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Vibanda vya Muda.”

Marejeo

  • +Kum 15:1
  • +Law 23:34

Kumbukumbu la Torati 31:11

Marejeo

  • +Kum 16:16
  • +Ne 8:7

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    3/15/2007, uku. 20

  • Fahirishi ya Machapisho

    w07 3/15 20

Kumbukumbu la Torati 31:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “watoto wachanga.”

  • *

    Tnn., “malango.”

Marejeo

  • +Kum 4:10; Ebr 10:25

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi (2010),

    4/15/2010, uku. 3

    9/15/2004, uku. 27

    3/15/2000, uku. 17

  • Fahirishi ya Machapisho

    w10 4/15 3; w04 9/15 27; w00 3/15 17

Kumbukumbu la Torati 31:13

Marejeo

  • +Kum 6:6, 7; Efe 6:4
  • +Kum 30:16

Kumbukumbu la Torati 31:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mchukue nafasi zenu.”

Marejeo

  • +Hes 27:13
  • +Kum 3:28

Kumbukumbu la Torati 31:15

Marejeo

  • +Kut 33:9; 40:38

Kumbukumbu la Torati 31:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kulala na baba zako.”

Marejeo

  • +Amu 2:17; Zb 106:37-39
  • +1Fa 11:33
  • +Amu 2:12, 20

Kumbukumbu la Torati 31:17

Marejeo

  • +Kum 29:20
  • +1Nya 28:9; 2Nya 15:2; 24:20
  • +Kum 32:20; Zb 104:29; Eze 39:23
  • +Ne 9:27
  • +Amu 6:13

Kumbukumbu la Torati 31:18

Marejeo

  • +Isa 59:2

Kumbukumbu la Torati 31:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Utieni katika vinywa vyao.”

Marejeo

  • +Kum 31:30; 32:44
  • +Kum 4:9; 11:19
  • +Kum 31:21

Kumbukumbu la Torati 31:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kunenepa.”

Marejeo

  • +Mwa 15:18
  • +Kut 3:8; Hes 13:26, 27
  • +Ne 9:25
  • +Kut 24:7; Kum 8:12-14; 29:1; Ne 9:26

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Kutoa Sababu, kur. 171-172

  • Fahirishi ya Machapisho

    rs 171-172

Kumbukumbu la Torati 31:21

Marejeo

  • +Kum 28:59
  • +Kut 16:4

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Ufahamu,

    Kutoa Sababu, kur. 171-172

  • Fahirishi ya Machapisho

    rs 171-172

Kumbukumbu la Torati 31:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaonekana ni Mungu.

Marejeo

  • +Hes 27:18; Kum 31:14
  • +Yos 1:6, 9
  • +Kum 1:38; 3:28

Kumbukumbu la Torati 31:24

Marejeo

  • +Kut 34:27

Kumbukumbu la Torati 31:26

Marejeo

  • +Kum 17:18; 2Nya 34:14
  • +1Fa 8:9

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    7/15/1990, uku. 28

Kumbukumbu la Torati 31:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “shingo yenu ngumu.”

Marejeo

  • +Kum 9:24; Ne 9:26
  • +Kut 32:9; Zb 78:8

Kumbukumbu la Torati 31:28

Marejeo

  • +Kum 30:19

Kumbukumbu la Torati 31:29

Marejeo

  • +Amu 2:19
  • +Kum 28:15

Kumbukumbu la Torati 31:30

Marejeo

  • +Kum 32:44

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

Kum. 31:2Kut 7:7; Kum 34:7; Mdo 7:23
Kum. 31:2Hes 20:12; Kum 3:27
Kum. 31:3Kum 9:3
Kum. 31:3Hes 27:18; Kum 3:28; Yos 1:2
Kum. 31:4Hes 21:23, 24
Kum. 31:4Hes 21:33, 35
Kum. 31:4Kut 23:23
Kum. 31:5Hes 33:52; Kum 7:2, 24; 20:16
Kum. 31:6Yos 1:6; Zb 27:14; 118:6
Kum. 31:6Hes 14:9; Kum 7:18
Kum. 31:6Kum 4:31; Yos 1:5; Ebr 13:5
Kum. 31:7Yos 10:25
Kum. 31:7Kum 1:38
Kum. 31:8Kut 33:14
Kum. 31:8Yos 1:9
Kum. 31:9Kut 34:27
Kum. 31:10Kum 15:1
Kum. 31:10Law 23:34
Kum. 31:11Kum 16:16
Kum. 31:11Ne 8:7
Kum. 31:12Kum 4:10; Ebr 10:25
Kum. 31:13Kum 6:6, 7; Efe 6:4
Kum. 31:13Kum 30:16
Kum. 31:14Hes 27:13
Kum. 31:14Kum 3:28
Kum. 31:15Kut 33:9; 40:38
Kum. 31:16Amu 2:17; Zb 106:37-39
Kum. 31:161Fa 11:33
Kum. 31:16Amu 2:12, 20
Kum. 31:17Kum 29:20
Kum. 31:171Nya 28:9; 2Nya 15:2; 24:20
Kum. 31:17Kum 32:20; Zb 104:29; Eze 39:23
Kum. 31:17Ne 9:27
Kum. 31:17Amu 6:13
Kum. 31:18Isa 59:2
Kum. 31:19Kum 31:30; 32:44
Kum. 31:19Kum 4:9; 11:19
Kum. 31:19Kum 31:21
Kum. 31:20Mwa 15:18
Kum. 31:20Kut 3:8; Hes 13:26, 27
Kum. 31:20Ne 9:25
Kum. 31:20Kut 24:7; Kum 8:12-14; 29:1; Ne 9:26
Kum. 31:21Kum 28:59
Kum. 31:21Kut 16:4
Kum. 31:23Hes 27:18; Kum 31:14
Kum. 31:23Yos 1:6, 9
Kum. 31:23Kum 1:38; 3:28
Kum. 31:24Kut 34:27
Kum. 31:26Kum 17:18; 2Nya 34:14
Kum. 31:261Fa 8:9
Kum. 31:27Kum 9:24; Ne 9:26
Kum. 31:27Kut 32:9; Zb 78:8
Kum. 31:28Kum 30:19
Kum. 31:29Amu 2:19
Kum. 31:29Kum 28:15
Kum. 31:30Kum 32:44
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Kumbukumbu la Torati 31:1-30

Kumbukumbu la Torati

31 Ndipo Musa akatoka na kuwaambia Waisraeli wote maneno haya: 2 “Leo nina umri wa miaka 120.+ Siwezi tena kuwaongoza,* kwa sababu Yehova ameniambia, ‘Hutavuka mto huu wa Yordani.’+ 3 Yehova Mungu wenu ndiye anayevuka mbele yenu, naye mwenyewe atayaangamiza mataifa haya kutoka mbele yenu, nanyi mtayafukuza.+ Yoshua ndiye atakayewaongoza kuvuka,+ kama Yehova alivyosema. 4 Yehova atayatendea kama alivyowatendea Sihoni+ na Ogu,+ wafalme wa Waamori, na nchi yao, alipowaangamiza.+ 5 Yehova atawashinda kwa niaba yenu, mtawatendea kulingana na amri yote ambayo nimewapa.+ 6 Iweni jasiri na imara.+ Msiogope wala msiwe na hofu mbele yao,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu ndiye anayepiga mwendo pamoja nanyi. Hatawatupa wala kuwaacha.”+

7 Kisha Musa akamwita Yoshua na kumwambia hivi mbele ya Waisraeli wote: “Uwe jasiri na imara,+ kwa sababu ni wewe utakayewaingiza watu hawa katika nchi ambayo Yehova aliwaapia mababu zao kwamba atawapa, nawe utawapa iwe urithi wao.+ 8 Yehova ndiye anayepiga mwendo mbele yako, naye ataendelea kuwa pamoja nawe.+ Hatakutupa wala kukuacha. Usiogope wala usihofu.”+

9 Ndipo Musa akaandika Sheria hii+ na kuwapa makuhani, Walawi, ambao wanabeba sanduku la agano la Yehova, na wazee wote wa Israeli. 10 Musa akawaamuru hivi: “Mwishoni mwa kila miaka saba, wakati uliowekwa katika mwaka wa kufuta madeni,+ wakati wa Sherehe ya Vibanda,*+ 11 Waisraeli wote wanapokuja mbele za Yehova+ Mungu wao mahali anapochagua, unapaswa kuisoma Sheria hii mbele ya Waisraeli wote ili waisikie.+ 12 Wakusanye watu pamoja,+ wanaume, wanawake, watoto,* na mkaaji mgeni aliye katika majiji* yenu, ili wasikilize na kujifunza kumhusu Yehova Mungu wenu na kumwogopa yeye na kuwa waangalifu kutekeleza maneno yote ya Sheria hii. 13 Ndipo wana wao ambao hawajui Sheria hii watasikiliza+ na kujifunza kumwogopa Yehova Mungu wenu sikuzote ambazo mtaishi katika nchi ambayo mnavuka Yordani kuimiliki.”+

14 Kisha Yehova akamwambia Musa, “Tazama! Wakati wako wa kufa umekaribia.+ Mwite Yoshua, nanyi mwende* kwenye hema la mkutano, ili nimweke yeye kuwa kiongozi.”+ Basi Musa na Yoshua wakaenda na kusimama kwenye hema la mkutano. 15 Ndipo Yehova akatokea pale hemani katika nguzo ya wingu, na nguzo hiyo ya wingu ikasimama karibu na mlango wa hema.+

16 Sasa Yehova akamwambia Musa hivi: “Tazama! Unakaribia kufa,* na watu hawa wataanza kufanya ukahaba wa kiroho pamoja na miungu ya kigeni inayowazunguka katika nchi wanayoenda.+ Wataniacha na kuvunja agano langu+ ambalo nimefanya pamoja nao.+ 17 Wakati huo hasira yangu itawaka dhidi yao,+ nami nitawaacha+ na kuuficha uso wangu wasiuone+ mpaka watakapoangamia. Kisha baada ya kupatwa na misiba na mateso mengi,+ watasema, ‘Je, hatujapatwa na misiba hii kwa sababu Mungu wetu hayuko miongoni mwetu?’+ 18 Lakini nitaendelea kuuficha uso wangu siku hiyo kwa sababu ya maovu yote waliyotenda kwa kuigeukia miungu mingine.+

19 “Sasa jiandikieni wimbo huu+ na kuwafundisha Waisraeli.+ Hakikisheni kwamba wanajifunza wimbo huu* ili uwe ushahidi wangu dhidi ya Waisraeli.+ 20 Nitakapowaleta katika nchi ambayo niliwaapia mababu zao+—nchi inayotiririka maziwa na asali+—nao wale na kushiba na kufanikiwa,*+ wataigeukia miungu mingine na kuiabudu na kunidharau na kulivunja agano langu.+ 21 Watakapopatwa na misiba na mateso mengi,+ wimbo huu utakuwa ushahidi kwao (kwa sababu wazao wao hawapaswi kuusahau), kwa sababu tayari ninajua mwelekeo ambao wamesitawisha+ hata kabla sijawaingiza katika nchi niliyowaapia.”

22 Basi Musa akaandika wimbo huu siku hiyo na kuwafundisha Waisraeli kuuimba.

23 Kisha akamweka* Yoshua+ mwana wa Nuni kuwa kiongozi na kusema: “Uwe jasiri na imara,+ kwa sababu ni wewe utakayewaingiza Waisraeli katika nchi ambayo nimewaapia,+ nami nitaendelea kuwa pamoja nawe.”

24 Mara tu Musa alipomaliza kuandika maneno yote ya Sheria hii katika kitabu,+ 25 Musa akawaamuru hivi Walawi wanaobeba sanduku la agano la Yehova: 26 “Chukueni kitabu hiki cha Sheria+ mkiweke kando ya sanduku+ la agano la Yehova Mungu wenu, nacho kitakuwa ushahidi dhidi yenu mahali hapo. 27 Kwa maana mimi mwenyewe najua vizuri uasi wenu+ na ukaidi wenu.*+ Ikiwa mmekuwa mkimwasi sana Yehova ningali hai pamoja nanyi, basi mtamwasi kadiri gani nikifa? 28 Nikusanyieni wazee wote wa makabila yenu na maofisa wenu, acheni niwaambie maneno haya wasikie, na acheni nichukue mbingu na dunia ziwe mashahidi dhidi yao.+ 29 Kwa maana najua vizuri kwamba baada ya kifo changu hakika mtatenda maovu+ na kuacha njia ambayo nimewaamuru ninyi. Na bila shaka mtapatwa na msiba+ siku zijazo, kwa sababu mtatenda maovu machoni pa Yehova, nanyi mtamkasirisha kwa kazi za mikono yenu.”

30 Kisha mbele ya Waisraeli wote, Musa akasema maneno ya wimbo huu kuanzia mwanzo mpaka mwisho:+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki