Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Mambo ya Nyakati 17
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

1 Mambo ya Nyakati—Yaliyomo

      • Daudi hatajenga hekalu (1-6)

      • Agano pamoja na Daudi kwa ajili ya ufalme (7-15)

      • Sala ya Daudi ya shukrani (16-27)

1 Mambo ya Nyakati 17:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “jumba lake mwenyewe la mfalme.”

Marejeo

  • +1Fa 1:8; 1Nya 29:29
  • +1Nya 14:1
  • +2Sa 7:1-3; 1Nya 15:1; 2Nya 1:4

1 Mambo ya Nyakati 17:4

Marejeo

  • +2Sa 7:4-7; 1Fa 8:17-19; 1Nya 22:7, 8

1 Mambo ya Nyakati 17:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Labda inamaanisha “kutoka kambi moja ya mahema hadi nyingine na kutoka eneo moja la kuishi hadi lingine.”

Marejeo

  • +Kut 40:2; Hes 4:24, 25; 2Sa 6:17; Zb 78:60

1 Mambo ya Nyakati 17:7

Marejeo

  • +1Sa 16:11, 12; 17:15; 25:30; 2Sa 7:8-11; Zb 78:70, 71

1 Mambo ya Nyakati 17:8

Marejeo

  • +1Sa 18:14; 2Sa 8:6
  • +1Sa 25:29; 26:10; Zb 89:20, 22
  • +1Sa 18:30

1 Mambo ya Nyakati 17:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “hawatawachosha.”

Marejeo

  • +Kut 2:23

1 Mambo ya Nyakati 17:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ukoo wa kifalme.”

Marejeo

  • +Amu 2:16
  • +Zb 18:40

1 Mambo ya Nyakati 17:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nitainua mbegu yako.”

Marejeo

  • +1Fa 8:20; Zb 132:11
  • +2Sa 7:12-17; 1Fa 9:5; 1Nya 28:5; Yer 23:5

1 Mambo ya Nyakati 17:12

Marejeo

  • +1Fa 5:5; 1Nya 22:10
  • +Zb 89:3, 4; Isa 9:7; Da 2:44

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Ulimwengu Usio na Vita, kur. 12-13

1 Mambo ya Nyakati 17:13

Marejeo

  • +2Sa 7:14; Lu 9:35; Ebr 1:5
  • +Isa 55:3
  • +1Sa 15:24, 28; 1Nya 10:13, 14

1 Mambo ya Nyakati 17:14

Marejeo

  • +Da 2:44; Yoh 1:49; 2Pe 1:11
  • +Zb 89:36; Yer 33:20, 21; Lu 1:32, 33; Ebr 1:8; Ufu 3:21

1 Mambo ya Nyakati 17:16

Marejeo

  • +2Sa 7:8, 18-20

1 Mambo ya Nyakati 17:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mtu mwenye cheo kikubwa.”

Marejeo

  • +Mt 22:42; Mdo 13:34; Ufu 22:16

1 Mambo ya Nyakati 17:18

Marejeo

  • +Zb 139:1

1 Mambo ya Nyakati 17:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kulingana na mapenzi yako.”

Marejeo

  • +2Sa 7:21-24

1 Mambo ya Nyakati 17:20

Marejeo

  • +Kut 15:11
  • +Isa 43:10

1 Mambo ya Nyakati 17:21

Marejeo

  • +Kum 4:7; Zb 147:20
  • +Kut 19:5; Zb 77:15
  • +Kum 4:34; Ne 9:10; Isa 63:12; Eze 20:9
  • +Kum 7:1; Yos 10:42; 21:44

1 Mambo ya Nyakati 17:22

Marejeo

  • +1Sa 12:22
  • +Mwa 17:7; Kum 7:6, 9

1 Mambo ya Nyakati 17:23

Marejeo

  • +2Sa 7:25-29

1 Mambo ya Nyakati 17:24

Marejeo

  • +2Nya 6:33; Zb 72:19; Mt 6:9; Yoh 12:28
  • +Zb 89:35, 36

1 Mambo ya Nyakati 17:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ukoo wa kifalme.”

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

1 Nya. 17:11Fa 1:8; 1Nya 29:29
1 Nya. 17:11Nya 14:1
1 Nya. 17:12Sa 7:1-3; 1Nya 15:1; 2Nya 1:4
1 Nya. 17:42Sa 7:4-7; 1Fa 8:17-19; 1Nya 22:7, 8
1 Nya. 17:5Kut 40:2; Hes 4:24, 25; 2Sa 6:17; Zb 78:60
1 Nya. 17:71Sa 16:11, 12; 17:15; 25:30; 2Sa 7:8-11; Zb 78:70, 71
1 Nya. 17:81Sa 18:14; 2Sa 8:6
1 Nya. 17:81Sa 25:29; 26:10; Zb 89:20, 22
1 Nya. 17:81Sa 18:30
1 Nya. 17:9Kut 2:23
1 Nya. 17:10Amu 2:16
1 Nya. 17:10Zb 18:40
1 Nya. 17:111Fa 8:20; Zb 132:11
1 Nya. 17:112Sa 7:12-17; 1Fa 9:5; 1Nya 28:5; Yer 23:5
1 Nya. 17:121Fa 5:5; 1Nya 22:10
1 Nya. 17:12Zb 89:3, 4; Isa 9:7; Da 2:44
1 Nya. 17:132Sa 7:14; Lu 9:35; Ebr 1:5
1 Nya. 17:13Isa 55:3
1 Nya. 17:131Sa 15:24, 28; 1Nya 10:13, 14
1 Nya. 17:14Da 2:44; Yoh 1:49; 2Pe 1:11
1 Nya. 17:14Zb 89:36; Yer 33:20, 21; Lu 1:32, 33; Ebr 1:8; Ufu 3:21
1 Nya. 17:162Sa 7:8, 18-20
1 Nya. 17:17Mt 22:42; Mdo 13:34; Ufu 22:16
1 Nya. 17:18Zb 139:1
1 Nya. 17:192Sa 7:21-24
1 Nya. 17:20Kut 15:11
1 Nya. 17:20Isa 43:10
1 Nya. 17:21Kum 4:7; Zb 147:20
1 Nya. 17:21Kut 19:5; Zb 77:15
1 Nya. 17:21Kum 4:34; Ne 9:10; Isa 63:12; Eze 20:9
1 Nya. 17:21Kum 7:1; Yos 10:42; 21:44
1 Nya. 17:221Sa 12:22
1 Nya. 17:22Mwa 17:7; Kum 7:6, 9
1 Nya. 17:232Sa 7:25-29
1 Nya. 17:242Nya 6:33; Zb 72:19; Mt 6:9; Yoh 12:28
1 Nya. 17:24Zb 89:35, 36
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
1 Mambo ya Nyakati 17:1-27

Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati

17 Mara tu Daudi alipoanza kuishi katika nyumba yake mwenyewe,* alimwambia hivi nabii Nathani:+ “Mimi hapa ninaishi katika nyumba ya mierezi+ huku sanduku la agano la Yehova likiwa ndani ya vitambaa vya mahema.”+ 2 Nathani akamwambia Daudi: “Fanya jambo lolote lililo moyoni mwako, kwa sababu Mungu wa kweli yuko pamoja nawe.”

3 Usiku huohuo, neno hili la Mungu likamjia Nathani: 4 “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Si wewe utakayenijengea nyumba nitakayokaa ndani yake.+ 5 Kwa maana sijakaa ndani ya nyumba tangu siku nilipowatoa nje Waisraeli mpaka leo, bali nimekuwa nikihama hema moja hadi hema lingine na kutoka hema moja la ibada hadi hema lingine la ibada.*+ 6 Wakati wote nilipotembea na Waisraeli wote, je, niliwahi wakati wowote kumuuliza mwamuzi yeyote wa Israeli niliyemweka awachunge watu wangu, ‘Kwa nini hukunijengea nyumba ya mierezi?’”’

7 “Sasa mwambie hivi mtumishi wangu Daudi: ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Nilikutoa malishoni, ili usiendelee kuchunga kondoo, uwe kiongozi wa watu wangu Waisraeli.+ 8 Nami nitakuwa pamoja nawe popote utakapoenda,+ nami nitawaangamiza maadui wako wote kutoka mbele yako;+ nami nitakujengea jina kama jina la watu maarufu duniani.+ 9 Nitachagua mahali kwa ajili ya watu wangu Waisraeli na kuwaweka humo, nao wataishi humo na hawatasumbuliwa tena; na watu waovu hawatawakandamiza* tena kama walivyofanya zamani,+ 10 tangu siku nilipowaweka waamuzi juu ya watu wangu Waisraeli.+ Nami nitawashinda maadui wako wote.+ Pia, ninakuambia, ‘Yehova atakujengea nyumba.’*

11 “‘“Siku zako zitakapokwisha nawe uzikwe pamoja na mababu zako, nitamwinua mzao wako* baada yako, mmoja wa wana wako,+ nami nitauimarisha kabisa ufalme wake.+ 12 Yeye ndiye atakayenijengea nyumba,+ nami nitakiimarisha kabisa kiti chake cha ufalme milele.+ 13 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu.+ Sitauondoa upendo wangu mshikamanifu kutoka kwake+ kama nilivyouondoa kutoka kwa yule aliyekutangulia.+ 14 Nitamfanya asimame katika nyumba yangu na katika ufalme wangu milele,+ na kiti chake cha ufalme kitadumu milele.”’”+

15 Nathani alimwambia Daudi maneno hayo yote na maono hayo yote.

16 Ndipo Mfalme Daudi akaingia na kuketi mbele za Yehova na kusema: “Mimi ni nani, Ee Yehova Mungu? Na nyumba yangu ni nini hivi kwamba umenileta mpaka hapa nilipofika?+ 17 Na kana kwamba hilo halitoshi, Ee Mungu, unasema pia kwamba nyumba yangu mimi mtumishi wako itadumu kwa muda mrefu,+ nawe umeniona kuwa mtu anayepaswa kukwezwa zaidi,* Ee Yehova Mungu. 18 Mimi mtumishi wako Daudi nitakwambia nini zaidi kuhusu heshima uliyonipa na wewe unanijua vizuri sana mimi mtumishi wako?+ 19 Ee Yehova, kwa ajili yangu mimi mtumishi wako na kupatana na moyo wako* umetenda mambo haya yote makuu kwa kufunua ukuu wako.+ 20 Ee Yehova, hakuna aliye kama wewe,+ na hakuna Mungu ila wewe;+ mambo yote tuliyosikia kwa masikio yetu yanathibitisha jambo hilo. 21 Na kuna taifa gani lingine duniani lililo kama watu wako Waisraeli?+ Wewe Mungu wa kweli ulienda na kuwakomboa wakiwa watu wako.+ Ulijijengea jina kwa matendo yako makuu na yenye kuogopesha,+ ukayafukuza mataifa kutoka mbele ya watu wako+ uliowakomboa kutoka Misri. 22 Uliwafanya watu wako Waisraeli wawe watu wako milele;+ na wewe, Ee Yehova, ukawa Mungu wao.+ 23 Sasa, Ee Yehova, ahadi uliyotoa kunihusu mimi mtumishi wako na nyumba yangu na ithibitike kuwa ya uaminifu milele, na ufanye kama ulivyoahidi.+ 24 Jina lako na lidumu na kukwezwa+ milele, ili watu waseme, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, ni Mungu kwa Israeli,’ na nyumba yangu mimi mtumishi wako Daudi na iimarishwe kabisa mbele zako.+ 25 Kwa maana wewe, Mungu wangu, umenifunulia mimi mtumishi wako kusudi lako la kunijengea nyumba.* Ndiyo sababu mimi mtumishi wako nina ujasiri wa kutoa sala hii kwako. 26 Na sasa, Ee Yehova, wewe ndiye Mungu wa kweli, nawe umeahidi mambo hayo mema kunihusu mimi mtumishi wako. 27 Basi na ufurahie kuibariki nyumba yangu mimi mtumishi wako, na idumu milele mbele zako, kwa sababu wewe, Ee Yehova, umeibariki, nayo imebarikiwa milele.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki