Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 17
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Wafalme—Yaliyomo

      • Hoshea, mfalme wa Israeli (1-4)

      • Kuanguka kwa Israeli (5, 6)

      • Waisraeli wapelekwa uhamishoni kwa sababu ya uasi imani (7-23)

      • Wageni waletwa katika majiji ya Samaria (24-26)

      • Mchanganyiko wa dini katika Samaria (27-41)

2 Wafalme 17:1

Marejeo

  • +2Fa 15:30

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    “Kila Andiko,” kur. 148-149

2 Wafalme 17:3

Marejeo

  • +2Fa 18:9; Isa 10:5, 6; Ho. 10:14, 15
  • +2Fa 18:14

2 Wafalme 17:4

Marejeo

  • +Isa 31:1

2 Wafalme 17:5

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    2/15/1988, uku. 27

2 Wafalme 17:6

Marejeo

  • +Ho. 13:16
  • +Law 26:32, 33; Kum 4:27; 28:64; 1Fa 14:15
  • +1Nya 5:26
  • +2Fa 18:9-11

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    “Kila Andiko,” kur. 145, 156

    Neno la Mungu, kur. 47-48

    Mnara wa Mlinzi,

    2/15/1988, uku. 27

2 Wafalme 17:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Waliogopa.”

Marejeo

  • +Kut 20:2
  • +Kut 20:5

2 Wafalme 17:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, kila mahali, penye watu wengi au wachache.

Marejeo

  • +Ho. 12:11

2 Wafalme 17:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Kut 34:13; Kum 16:21, 22
  • +Kum 12:2; Isa 57:5

2 Wafalme 17:11

Marejeo

  • +Law 20:23

2 Wafalme 17:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.

Marejeo

  • +1Fa 12:28-30; 21:25, 26
  • +Kut 20:3-5; Law 26:1; Kum 4:23

2 Wafalme 17:13

Marejeo

  • +2Nya 24:18, 19; 36:15, 16; Yer 25:4
  • +Isa 55:7

2 Wafalme 17:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kufanya shingo zao kuwa ngumu kama shingo za.”

Marejeo

  • +Kum 1:32; 31:27

2 Wafalme 17:15

Marejeo

  • +Kum 5:2; 29:12
  • +Ho. 4:6
  • +Kum 32:21; 1Sa 12:21
  • +Zb 115:4-8; Isa 44:9
  • +Kum 12:30

2 Wafalme 17:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “za kuyeyushwa.”

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +1Fa 12:28-30
  • +1Fa 14:15; 16:33
  • +Kum 4:19; Yer 8:2
  • +1Fa 16:30, 31; 22:51, 53; 2Fa 10:21; 23:4, 5

2 Wafalme 17:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “waliwapitisha.”

  • *

    Au “wakabashiri.”

  • *

    Tnn., “kujiuza.”

Marejeo

  • +2Fa 16:1, 3
  • +Kum 18:10; Mik 5:12

2 Wafalme 17:18

Marejeo

  • +Yos 23:12, 13; Isa 42:24

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    “Kila Andiko,” uku. 145

2 Wafalme 17:19

Marejeo

  • +1Fa 14:22; Yer 3:8
  • +Eze 23:4, 11

2 Wafalme 17:21

Marejeo

  • +1Fa 12:20

2 Wafalme 17:22

Marejeo

  • +1Fa 12:28-30

2 Wafalme 17:23

Marejeo

  • +Kum 28:45, 63; 1Fa 14:16; Ho. 1:4; Amo 5:27; Mik 1:6
  • +2Fa 18:11

2 Wafalme 17:24

Marejeo

  • +2Fa 19:11, 13

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    2/15/1988, uku. 27

2 Wafalme 17:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hawakumwabudu.”

Marejeo

  • +Kut 23:29

2 Wafalme 17:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hayajui desturi za dini.”

2 Wafalme 17:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kumwabudu.”

Marejeo

  • +Mwa 28:18, 19; Yos 16:1; 1Fa 12:28, 29
  • +Yoh 4:20-22

2 Wafalme 17:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “miungu yake na kuiweka.”

2 Wafalme 17:30

Marejeo

  • +2Fa 17:24

2 Wafalme 17:31

Marejeo

  • +2Fa 18:34

2 Wafalme 17:32

Marejeo

  • +1Fa 12:31, 32; 13:33

2 Wafalme 17:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “desturi za dini.”

Marejeo

  • +2Fa 17:24, 41

2 Wafalme 17:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “desturi za dini.”

  • *

    Tnn., “anayemwogopa.”

Marejeo

  • +Mwa 32:28

2 Wafalme 17:35

Marejeo

  • +Kut 19:5; 24:7; Kum 29:1
  • +Kut 20:3-5; 23:24; 34:14; Kum 5:9

2 Wafalme 17:36

Marejeo

  • +Kut 6:6
  • +Kum 6:12, 13

2 Wafalme 17:37

Marejeo

  • +Kum 31:9

2 Wafalme 17:38

Marejeo

  • +Kum 4:23

2 Wafalme 17:40

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “desturi za dini.”

Marejeo

  • +2Fa 17:34

2 Wafalme 17:41

Marejeo

  • +Ezr 4:1, 2

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    12/1/1990, uku. 3

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

2 Fal. 17:12Fa 15:30
2 Fal. 17:32Fa 18:9; Isa 10:5, 6; Ho. 10:14, 15
2 Fal. 17:32Fa 18:14
2 Fal. 17:4Isa 31:1
2 Fal. 17:6Ho. 13:16
2 Fal. 17:6Law 26:32, 33; Kum 4:27; 28:64; 1Fa 14:15
2 Fal. 17:61Nya 5:26
2 Fal. 17:62Fa 18:9-11
2 Fal. 17:7Kut 20:2
2 Fal. 17:7Kut 20:5
2 Fal. 17:9Ho. 12:11
2 Fal. 17:10Kut 34:13; Kum 16:21, 22
2 Fal. 17:10Kum 12:2; Isa 57:5
2 Fal. 17:11Law 20:23
2 Fal. 17:121Fa 12:28-30; 21:25, 26
2 Fal. 17:12Kut 20:3-5; Law 26:1; Kum 4:23
2 Fal. 17:132Nya 24:18, 19; 36:15, 16; Yer 25:4
2 Fal. 17:13Isa 55:7
2 Fal. 17:14Kum 1:32; 31:27
2 Fal. 17:15Kum 5:2; 29:12
2 Fal. 17:15Ho. 4:6
2 Fal. 17:15Kum 32:21; 1Sa 12:21
2 Fal. 17:15Zb 115:4-8; Isa 44:9
2 Fal. 17:15Kum 12:30
2 Fal. 17:161Fa 12:28-30
2 Fal. 17:161Fa 14:15; 16:33
2 Fal. 17:16Kum 4:19; Yer 8:2
2 Fal. 17:161Fa 16:30, 31; 22:51, 53; 2Fa 10:21; 23:4, 5
2 Fal. 17:172Fa 16:1, 3
2 Fal. 17:17Kum 18:10; Mik 5:12
2 Fal. 17:18Yos 23:12, 13; Isa 42:24
2 Fal. 17:191Fa 14:22; Yer 3:8
2 Fal. 17:19Eze 23:4, 11
2 Fal. 17:211Fa 12:20
2 Fal. 17:221Fa 12:28-30
2 Fal. 17:23Kum 28:45, 63; 1Fa 14:16; Ho. 1:4; Amo 5:27; Mik 1:6
2 Fal. 17:232Fa 18:11
2 Fal. 17:242Fa 19:11, 13
2 Fal. 17:25Kut 23:29
2 Fal. 17:28Mwa 28:18, 19; Yos 16:1; 1Fa 12:28, 29
2 Fal. 17:28Yoh 4:20-22
2 Fal. 17:302Fa 17:24
2 Fal. 17:312Fa 18:34
2 Fal. 17:321Fa 12:31, 32; 13:33
2 Fal. 17:332Fa 17:24, 41
2 Fal. 17:34Mwa 32:28
2 Fal. 17:35Kut 19:5; 24:7; Kum 29:1
2 Fal. 17:35Kut 20:3-5; 23:24; 34:14; Kum 5:9
2 Fal. 17:36Kut 6:6
2 Fal. 17:36Kum 6:12, 13
2 Fal. 17:37Kum 31:9
2 Fal. 17:38Kum 4:23
2 Fal. 17:402Fa 17:34
2 Fal. 17:41Ezr 4:1, 2
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
2 Wafalme 17:1-41

Kitabu cha Pili cha Wafalme

17 Katika mwaka wa 12 wa utawala wa Mfalme Ahazi wa Yuda, Hoshea+ mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli huko Samaria; alitawala kwa miaka tisa. 2 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, lakini si kwa kiwango ambacho wafalme wa Israeli waliomtangulia walitenda. 3 Mfalme Shalmanesa wa Ashuru alipanda kuja kumshambulia,+ na Hoshea akawa mtumishi wake, akaanza kumlipa ushuru.+ 4 Hata hivyo, mfalme wa Ashuru alipata habari kwamba Hoshea alishiriki kupanga njama fulani, kwa maana alikuwa amewatuma wajumbe kwa Mfalme So wa Misri+ na hakuleta ushuru kwa mfalme wa Ashuru kama alivyofanya miaka iliyotangulia. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akamfunga na kumtia gerezani.

5 Mfalme wa Ashuru aliivamia nchi nzima, naye akaja Samaria na kulizingira kwa miaka mitatu. 6 Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mfalme wa Ashuru aliliteka jiji la Samaria.+ Kisha akawapeleka Waisraeli uhamishoni+ kule Ashuru na kuwaweka katika eneo la Hala na Habori kando ya mto Gozani+ na katika majiji ya Wamedi ili waishi humo.+

7 Hilo lilitendeka kwa sababu Waisraeli walimtendea dhambi Yehova Mungu wao, aliyewatoa nchini Misri kutoka mikononi mwa Farao mfalme wa Misri.+ Waliabudu* miungu mingine,+ 8 wakafuata desturi za mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli, nao wakafuata desturi zilizoanzishwa na wafalme wa Israeli.

9 Waisraeli walikuwa wakifuatia mambo ambayo hayakuwa sawa machoni pa Yehova Mungu wao. Wakaendelea kujenga mahali pa juu katika majiji yao yote,+ kuanzia mnara wa walinzi mpaka jiji lenye ngome.* 10 Wakaendelea kujisimamishia nguzo takatifu na miti mitakatifu*+ juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti wenye majani mengi;+ 11 nao walikuwa wakifukiza moshi wa dhabihu mahali pote pa juu kama yalivyofanya mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyapeleka uhamishoni kutoka mbele yao.+ Waliendelea kutenda maovu na kumkasirisha Yehova.

12 Waliendelea kuabudu sanamu zenye kuchukiza,*+ ambazo Yehova alikuwa amewaambia hivi kuzihusu: “Msifanye hivyo!”+ 13 Yehova aliwaonya Waisraeli na watu wa Yuda tena na tena kupitia manabii wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni na kuacha njia zenu ovu!+ Shikeni amri zangu na maagizo yangu kulingana na sheria yote niliyowaamuru mababu zenu na ambayo niliwapa kupitia watumishi wangu manabii.” 14 Lakini hawakusikiliza, nao wakaendelea kuwa wakaidi kama* mababu zao ambao hawakudhihirisha imani katika Yehova Mungu wao.+ 15 Waliendelea kukataa masharti yake na agano lake+ alilofanya na mababu zao na vikumbusho vyake alivyowapa ili kuwaonya,+ nao wakaendelea kufuata sanamu za ubatili,+ na wao wenyewe wakawa ubatili,+ wakiiga mataifa yaliyowazunguka pande zote ambayo Yehova alikuwa amewaamuru wasiyaige.+

16 Waliendelea kuacha amri zote za Yehova Mungu wao, nao wakatengeneza sanamu za chuma* za ndama wawili+ na kutengeneza mti mtakatifu,*+ nao wakaliinamia jeshi lote la mbinguni+ na kumwabudu Baali.+ 17 Pia waliwateketeza* motoni wana wao na mabinti wao,+ wakafanya uaguzi,*+ wakatafuta ishara za ubashiri, na wakaendelea kujitoa* wenyewe kutenda maovu machoni pa Yehova, na kumkasirisha.

18 Kwa hiyo Yehova akawakasirikia sana Waisraeli hivi kwamba akawaondoa mbele zake.+ Hakumwacha yeyote abaki isipokuwa watu wa kabila la Yuda peke yao.

19 Hata watu wa kabila la Yuda hawakushika amri za Yehova Mungu wao;+ walifuata pia desturi zilizofuatwa na Waisraeli.+ 20 Yehova aliwakataa wazao wote wa Israeli, akawaaibisha na kuwatia mikononi mwa waporaji, mpaka alipowatupa mbali kutoka mbele zake. 21 Aliwararua Waisraeli kutoka katika nyumba ya Daudi, nao wakamweka Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme.+ Lakini Yeroboamu akasababisha Waisraeli wapotoke na kuacha kumfuata Yehova, naye akasababisha watende dhambi kubwa. 22 Na Waisraeli wakaendelea kufuata dhambi zote ambazo Yeroboamu alitenda.+ Hawakuziacha 23 mpaka Yehova alipowaondoa Waisraeli kutoka mbele zake, kama alivyokuwa amesema kupitia watumishi wake wote manabii.+ Kwa hiyo Waisraeli wakaondolewa katika nchi yao na kupelekwa uhamishoni kule Ashuru,+ nao wangali huko hadi leo.

24 Kisha mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babiloni, Kutha, Ava, Hamathi, na Sefarvaimu+ na kuwaweka katika majiji ya Samaria ili waishi humo badala ya Waisraeli; nao wakamiliki Samaria na kuishi katika majiji yake. 25 Walipoanza kuishi humo, hawakumwogopa* Yehova. Kwa hiyo Yehova akawatuma simba waje miongoni mwao,+ nao wakawaua baadhi ya watu. 26 Mfalme wa Ashuru akapata habari hii: “Mataifa uliyoyapeleka uhamishoni na kuyaweka katika majiji ya Samaria ili yaishi humo hayajui dini* ya Mungu wa nchi hiyo. Kwa hiyo anaendelea kuwatuma simba miongoni mwao; na simba hao wanawaua, kwa sababu hakuna yeyote kati yao anayejua dini ya Mungu wa nchi hiyo.”

27 Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mrudisheni huko mmoja wa makuhani mliowaleta uhamishoni, aishi huko na kuwafundisha watu hao dini ya Mungu wa nchi hiyo.” 28 Basi mmoja wa makuhani ambao walikuwa wamepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akarudi na kuishi Betheli,+ naye akaanza kuwafundisha jinsi wanavyopaswa kumwogopa* Yehova.+

29 Hata hivyo, kila taifa likajitengenezea mungu wake na kumweka* katika nyumba za ibada mahali pa juu ambapo Wasamaria walikuwa wamejenga; kila taifa lilifanya hivyo katika majiji walimokuwa wakiishi. 30 Basi wanaume wa Babiloni wakatengeneza Sukoth-benothi, na wanaume wa Kuthi wakatengeneza Nergali, na wanaume wa Hamathi+ wakatengeneza Ashima, 31 na Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki. Wasefarvaimu walikuwa wakiwateketeza wana wao motoni kwa ajili ya Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.+ 32 Ingawa walimwogopa Yehova, waliwachagua makuhani kutoka kwa watu wa kawaida ili wahudumu mahali pa juu, na makuhani hao walihudumu kwa niaba yao mahali pa juu katika nyumba za ibada.+ 33 Kwa hiyo walimwogopa Yehova, lakini waliabudu miungu yao wenyewe kulingana na dini* ya mataifa ambamo walitolewa.+

34 Mpaka leo wanafuata dini* zao za awali. Hakuna yeyote kati yao anayemwabudu* Yehova, na hakuna yeyote anayefuata maagizo yake, hukumu zake, na Sheria, na amri ambayo Yehova aliwapa wana wa Yakobo, ambaye alibadili jina lake na kumwita Israeli.+ 35 Yehova alipofanya agano pamoja nao,+ aliwaamuru hivi: “Msiogope miungu mingine, wala msiiinamie wala kuiabudu wala kuitolea dhabihu.+ 36 Lakini mnapaswa kumwogopa Yehova, aliyewatoa nchini Misri kwa nguvu nyingi na kwa mkono ulionyooshwa,+ Yeye ndiye mnayepaswa kumwogopa,+ nanyi mnapaswa kumwinamia yeye, nanyi mnapaswa kumtolea yeye dhabihu. 37 Nanyi mnapaswa sikuzote kufuata kwa uangalifu masharti, maamuzi, Sheria, na amri aliyowaandikia,+ na hampaswi kuogopa miungu mingine. 38 Na hampaswi kusahau agano nililofanya pamoja nanyi,+ na hampaswi kuogopa miungu mingine. 39 Lakini mnapaswa kumwogopa Yehova Mungu wenu, kwa kuwa yeye ndiye atakayewaokoa kutoka mikononi mwa maadui wenu wote.”

40 Lakini hawakutii, nao wakafuata dini* yao ya awali.+ 41 Kwa hiyo mataifa hayo yakamwogopa Yehova,+ lakini yalikuwa pia yakiabudu sanamu zao za kuchongwa. Wana wao na wajukuu wao wamekuwa wakitenda kama mababu zao mpaka leo hii.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki