Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
TAARIFA: Kuanzia toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu, Ratiba ya Mkutano wa Utumishi itatia ndani muhtasari wa Mkutano wa Utumishi wa kwanza wa mwezi unaofuata. Rekebisho hilo limefanywa ili kulipia kucheleweshwa kwa upelekaji ambao huenda ukachelewa wa Huduma ya Ufalme Yetu.
Juma Linaloanza Desemba 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 15: “Iga Sifa ya Yehova ya Kutobagua.” Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Eleza maana ya kutobagua, jinsi ambavyo Yehova huonyesha sifa hiyo, na jinsi tunavyoweza kuionyesha katika huduma yetu.—Ona Insight, Buku la 1, ukurasa wa 1192, fungu la 4-7.
Dak. 20: “Je, Hatujapata Kuyasikia Hapo Awali?” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Omba wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo kurudia kumewasaidia waelewe na kuthamini kweli zaidi.—Ona Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1995, ukurasa wa 21-22, na Agosti 15, 1993, ukurasa wa 13-14, fungu la 10-12.
Wimbo 218 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 13
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Toa madokezo ya jinsi ya kuitikia kwa busara salamu za sikukuu. Ikiwa makutaniko yana nakala za kitabu Mtu Mkuu Zaidi au Mwalimu Mkuu akibani, onyesha jinsi zinavyoweza kutumiwa kwa manufaa katika huduma wakati wa sikukuu ya Krismasi.
Dak. 15: “Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2000.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Pitia mabadiliko yafuatayo katika ratiba ya mwaka mpya. Mgawo Na. 3 na Na. 4 utategemea “Vichwa vya Biblia vya Mazungumzo” kama vipatikanavyo katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Mahali ambapo kuna ishara ya namba (#) inapofuata mgawo huo, inapendekezwa kwamba ndugu agawiwe sehemu hiyo. Watie wote moyo waendelee na usomaji wao wa Biblia wa kila juma na kuwa wenye bidii kutimiza migawo ya shule.
Dak. 20: “Utamwambia Nini Mtu Asiyeamini Mungu?” Maswali na majibu. Chunguzeni sababu mbalimbali ambazo zimefanya wengi wakapoteza imani katika Mungu. Dokeza baadhi ya njia ambazo zaweza kutumiwa kuwafikia na kuwasaidia waone mantiki katika kutambua kuwapo kwa Mungu. Panga kuwe na onyesho moja au mawili mafupi. Ili upate habari zaidi ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 218-224, na kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, ukurasa wa 14.
Wimbo 220 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 20
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na “Ona Nguvu Iliyo Nayo Biblia!” Panga wahubiri wasimulie mambo yaliyoonwa mafupi hususa ambayo wamepata karibuni katika utumishi.
Dak. 15: Kuitikia Vizuia-Mazungumzo Vinavyoweza Kutokea. Mazungumzo na wasikilizaji na maonyesho. Soma “Maelezo” kwenye ukurasa wa 15-16 wa kitabu Kutoa Sababu. Chagua “Vizuia-Mazungumzo” viwili au vitatu kutoka ukurasa wa 16-20, au utumie vingine ambavyo hupatikana mara nyingi katika eneo lenu. Pitieni baadhi ya madokezo ya maitikio, na kuchanganua kwa nini huenda yakawa na matokeo katika eneo lenu. Toa wonyesho kifupi wa vichache kati ya hivyo. Waombe wasikilizaji wasimulie maitikio ambayo wametumia wakapata matokeo mazuri.
Dak. 20: Je, Nikubali Kazi ya Kuajiriwa Katika Shirika Linalohusika na Mambo ya Kidini? Hotuba itolewe na mzee, ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 1999, ukurasa wa 28-30. Watu fulani wamekubali kazi ya kuajiriwa kama hiyo na baadaye wakagundua kwamba kile walichokuwa wakifanya hakikupatana na kanuni za Biblia. Chunguzeni maswali ambayo tunahitaji kufikiria tunapofanya uamuzi wa kufanya kazi iliyo na uhusiano na mambo ya kidini. Tia moyo wote wafuatie mwendo utakaowahakikishia msimamo mzuri mbele za Yehova.—2 Kor. 6:3, 4, 14-18.
Wimbo 109 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 27
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kama kutaniko lenu litabadilisha saa za mikutano mwaka mpya, toa kitia-moyo ukiwasihi wote waendelee kuhudhuria mikutano kwa ukawaida katika saa mpya. Julisheni wanafunzi wa Biblia na wengine wanaopendezwa juu ya mabadiliko yoyote, na muanze kutumia vikaratasi vya kukaribisha watu vinavyoonyesha ratiba mpya. Wakumbushe wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Desemba.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: Kutoa Vitabu vya Zamani Mwezi wa Januari. Hotuba na maonyesho. Onyesha vitabu vya zamani viwili au vitatu vya kurasa 192, vilivyochapishwa kabla ya 1986, vilivyo katika akiba ya kutaniko, na utie moyo wahubiri wavichukue vingine kwa ajili ya huduma ya shambani. (Ikiwa havipatikani, zungumzia toleo la fasihi la badala la Januari.) Eleza sababu inayofanya vichapo hivi vya zamani viwe bado na matokeo katika kusitawisha kupendezwa katika Biblia. Katika kila kitabu kazia mambo makuu na picha zinazoweza kutumiwa vizuri ili kuanzisha mazungumzo. Toa wonyesho wa utoaji mmoja au maonyesho mawili. Mahali palipo na upendezi, broshua Anataka yaweza kutumiwa kuanzisha funzo.
Wimbo 224 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 3
Dak. 8: Matangazo ya kwenu.
Dak. 17: Jua Jinsi ya Kutoa Jibu. (Kol. 4:6) Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji. Kitabu Kutoa Sababu ni msaada mzuri zaidi katika kufungua njia ya kuwaambia wengine kweli ya Biblia. Mwenye nyumba akipinga mojawapo ya itikadi zetu, labda twaweza kutumia ile sehemu “Mtu Akisema—” mwishoni mwa sehemu inayoshughulika na itikadi hiyo. Zungumza juu ya maelezo kuhusu Biblia yaliyo kwenye ukurasa wa 46-49, na mchunguze kwa nini majibu yaliyodokezwa yanaweza kuwa yenye matokeo.
Dak. 20: “Mkusanyiko wa Wilaya wa 2000 wa ‘Watekelezaji wa Neno la Mungu’ wa Mashahidi wa Yehova.” Mwandishi ashughulikia makala hiyo ya nyongeza kwa maswali na majibu. Kwanza, soma barua ya mgawo wa mkusanyiko ya Desemba 15, 1999. Tumia maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa kuonyesha sababu ambayo sisi sote twahitaji kufuata sana mwelekezo wa Sosaiti. Kazia umuhimu wa kila mtu kufanya mipango hususa ya tarehe za likizo mapema zaidi ili kuhudhuria kila siku ya mkusanyiko, kutia ndani Ijumaa. Pongeza akina ndugu kwa kushirikiana na mipango ya Sosaiti.
Wimbo 56 na sala ya kumalizia.