1 Mambo ya Nyakati
27 Kwa habari ya wana wa Israeli kulingana na hesabu yao, walio vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba+ na wakuu+ wa maelfu na wa mamia+ na maofisa wao waliomhudumia+ mfalme katika kila jambo la ile migawanyo ya wale walioingia na kutoka mwezi kwa mwezi kwa miezi yote ya mwaka, katika kila mgawanyo kulikuwa na watu 24,000.
2 Juu ya mgawanyo wa kwanza wa mwezi wa kwanza kulikuwa na Yashobeamu+ mwana wa Zabdieli, na katika mgawanyo wake kulikuwa na watu 24,000. 3 Baadhi ya wana wa Perezi+ aliye kichwa cha wakuu wote wa vikundi vya utumishi walikuwa kwa ajili ya mwezi wa kwanza. 4 Na juu ya mgawanyo wa mwezi wa pili kulikuwa na Dodai+ Mwahohi+ na mgawanyo wake, na Miklothi ndiye aliyekuwa kiongozi, na katika mgawanyo wake kulikuwa na watu 24,000. 5 Mkuu wa kikundi cha tatu cha utumishi kwa ajili ya mwezi wa tatu alikuwa ni Benaya+ mwana wa Yehoyada+ mkuu wa makuhani, na katika mgawanyo wake kulikuwa na watu 24,000. 6 Huyo Benaya+ alikuwa mwanamume mwenye nguvu wa wale 30+ na juu ya wale 30; na juu ya mgawanyo wake kulikuwa na Amizabadi mwana wake. 7 Wa nne kwa ajili ya mwezi wa nne alikuwa Asaheli,+ ndugu ya Yoabu,+ na Zebadia mwana wake baada yake, na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 8 Mkuu wa tano kwa ajili ya mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi+ Mwizrahia, na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 9 Wa sita kwa ajili ya mwezi wa sita alikuwa Ira+ mwana wa Ikeshi+ Mtekoa,+ na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 10 Wa saba kwa ajili ya mwezi wa saba alikuwa Helezi+ Mpeloni,+ wa wana wa Efraimu, na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 11 Wa nane kwa ajili ya mwezi wa nane alikuwa Sibekai+ Mhusha wa Wazera,+ na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 12 Wa tisa kwa ajili ya mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri+ Mwanathothi+ wa Wabenyamini, na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 13 Wa kumi kwa ajili ya mwezi wa kumi alikuwa Maharai+ Mnetofa wa Wazera,+ na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 14 Wa kumi na moja kwa ajili ya mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya+ Mpirathoni wa wana wa Efraimu,+ na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 15 Wa kumi na mbili kwa ajili ya mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai+ Mnetofa, wa Othnieli, na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000.
16 Na juu ya makabila ya Israeli,+ wa Warubeni, Eliezeri mwana wa Zikri ndiye aliyekuwa kiongozi; wa Wasimeoni, Shefatia mwana wa Maaka; 17 wa Lawi, Hashabia mwana wa Kemueli; wa Haruni, Sadoki;+ 18 wa Yuda, Elihu,+ mmoja wa ndugu za Daudi;+ wa Isakari, Omri mwana wa Mikaeli; 19 wa Zabuloni, Ishmaya mwana wa Obadia; wa Naftali, Yerimothi mwana wa Azrieli; 20 wa wana wa Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia; wa nusu ya kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaya; 21 wa nusu ya kabila la Manase katika Gileadi, Ido mwana wa Zekaria; wa Benyamini, Yaasieli mwana wa Abneri;+ 22 wa Dani, Azareli mwana wa Yerohamu. Hao walikuwa wakuu+ wa makabila ya Israeli.
23 Na Daudi hakuhesabu wale waliokuwa na umri wa miaka 20 kurudi chini, kwa sababu Yehova alikuwa ameahidi kufanya Israeli kuwa wengi kama nyota za mbinguni.+ 24 Yoabu+ mwana wa Seruya alikuwa ameanza kuhesabu, lakini hakumaliza;+ na kwa sababu hiyo kukawa na ghadhabu+ juu ya Israeli, na hesabu hiyo haikuwekwa katika hesabu ya mambo ya siku za Mfalme Daudi.
25 Na juu ya hazina za mfalme+ kulikuwa na Azmavethi mwana wa Adieli. Na juu ya hazina katika shamba,+ katika majiji+ na katika vijiji na katika minara kulikuwa na Yonathani mwana wa Uzia. 26 Na juu ya wafanyakazi shambani,+ kwa ajili ya kulima udongo, kulikuwa na Ezri mwana wa Kelubu. 27 Na juu ya mashamba ya mizabibu+ kulikuwa na Shimei Mrama; na juu ya vitu vilivyokuwa katika mashamba ya mizabibu kwa ajili ya akiba za divai kulikuwa na Zabdi Mshifi. 28 Na juu ya mashamba ya mizeituni na mikuyu+ iliyokuwa katika Shefela+ kulikuwa na Baal-hanani Mgederi; na juu ya akiba ya mafuta+ kulikuwa na Yoashi. 29 Na juu ya mifugo iliyokuwa ikilisha katika Sharoni+ kulikuwa na Shitrai Msharoni; na juu ya mifugo katika nchi tambarare za chini kulikuwa na Shafati mwana wa Adlai. 30 Na juu ya ngamia+ kulikuwa na Obili Mwishmaeli;+ na juu ya punda-jike kulikuwa na Yehdeya Mmeronothi. 31 Na juu ya makundi kulikuwa na Yazizi Mhagri. Hao wote ndio waliokuwa wakuu wa mali za Mfalme Daudi.
32 Na Yonathani,+ mpwa wa Daudi, alikuwa mshauri, mwanamume mwenye uelewaji,+ naye alikuwa mwandishi pia; na Yehieli mwana wa Hakmoni+ alikuwa pamoja na wana wa mfalme.+ 33 Na Ahithofeli+ alikuwa mshauri+ wa mfalme; na Hushai+ Mwarki,+ alikuwa rafiki ya mfalme.+ 34 Na baada ya Ahithofeli kulikuwa na Yehoyada mwana wa Benaya+ na Abiathari;+ na Yoabu+ alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.