Zaburi
Ya Daudi. Muziki.
110 Neno la Yehova kwa Bwana wangu ni:+
“Keti kwenye mkono wangu wa kuume+
Mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako.”+
2 Yehova ataituma fimbo+ ya nguvu zako kutoka Sayuni,+ akisema:
“Nenda ukitiisha katikati ya adui zako.”+
3 Watu wako+ watajitoa kwa hiari+ katika siku ya jeshi lako.+
Katika fahari za utakatifu,+ kutoka tumbo la uzazi la mapambazuko,
Una kundi lako la vijana kama matone ya
umande.+
4 Yehova ameapa+ (naye hatajuta):+
“Wewe ni kuhani mpaka wakati usio na kipimo+
Kwa mfano wa Melkizedeki!”+
5 Yehova mwenyewe akiwa upande wako wa mkono wa kuume+
Hakika atawavunja vipande-vipande wafalme katika siku ya hasira yake.+