2 Wakorintho
2 Kwa maana hili ndilo nimejiamulia mwenyewe, nisije kwenu tena kwa huzuni.+ 2 Kwa maana nikiwahuzunisha ninyi,+ kwa kweli ni nani aliyeko wa kunichangamsha isipokuwa yeye ambaye mimi ninamhuzunisha? 3 Na kwa hiyo niliandika jambo hili, ili, nitakapokuja, nisihuzunike+ kwa sababu ya wale ambao ninapaswa kushangilia juu yao;+ kwa sababu nina uhakika+ katika ninyi nyote kwamba shangwe niliyo nayo ni ile yenu nyote. 4 Kwa maana kutokana na dhiki nyingi na maumivu makali ya moyo niliwaandikia ninyi kwa machozi mengi,+ si ili mhuzunishwe,+ bali ili muujue upendo nilio nao hasa zaidi kwa ajili yenu.
5 Basi ikiwa yeyote amesababisha huzuni,+ amehuzunisha, si mimi, bali ninyi nyote kwa kadiri fulani—nisiwe mkali mno kwa yale ninayosema. 6 Kemeo+ hili linalotolewa na walio wengi linamtosha mtu wa namna hiyo, 7 ili kwamba, kinyume chake sasa, mnapaswa kumsamehe+ kwa fadhili na kumfariji, ili kwa njia fulani mtu huyo asimezwe na huzuni yake ya kupita kiasi.+ 8 Kwa hiyo nawahimiza ninyi kumthibitishia upendo+ wenu. 9 Kwa maana kwa lengo hili pia ninaandika ili kuhakikisha uthibitisho wenu, kama ninyi ni watiifu katika mambo yote.+ 10 Jambo lolote ambalo mnamsamehe yeyote kwa fadhili, mimi vilevile namsamehe.+ Kwa kweli, kwa habari yangu mimi, lolote lile ambalo nimesamehe kwa fadhili, ikiwa nimesamehe kwa fadhili jambo lolote, imekuwa ni kwa ajili yenu machoni pa Kristo; 11 ili Shetani+ asitushinde akili, kwa maana sisi hatukosi kuzijua mbinu zake.+
12 Basi nilipofika Troa+ kutangaza habari njema juu ya Kristo, nami nikafunguliwa mlango katika Bwana,+ 13 sikupata kitulizo katika roho yangu kwa sababu ya kukosa kumkuta Tito+ ndugu yangu, bali niliwaaga kisha nikaondoka kwenda Makedonia.+
14 Lakini Mungu apewe shukrani, ambaye sikuzote hutuongoza+ katika maandamano yenye shangwe ya ushindi kwa kushirikiana+ na Kristo naye huifanya harufu ya ujuzi juu yake yeye ifahamike kupitia sisi kila mahali!+ 15 Kwa maana kwa Mungu sisi ni harufu tamu+ ya Kristo katikati ya wale wanaookolewa na katikati ya wale wanaoangamia;+ 16 kwa hawa wa mwisho ni harufu inayotoka katika kifo mpaka kifo,+ kwa wale wa kwanza ni harufu inayotoka katika uzima mpaka uzima. Na ni nani ambaye ana sifa za kustahili vya kutosha kwa ajili ya mambo haya?+ 17 Ni sisi; kwa maana sisi si wachuuzi wa neno la Mungu+ kama watu wengi walivyo,+ bali tunasema kwa unyoofu wa moyo, ndiyo, tukiwa waliotumwa kutoka kwa Mungu, machoni pa Mungu, kwa kushirikiana na Kristo.+