1 Samweli
29 Na Wafilisti+ wakakusanya kambi zao zote kule Afeki, huku Waisraeli wakipiga kambi kando ya bubujiko lililo katika Yezreeli.+ 2 Na wakuu wa muungano wa Wafilisti+ walikuwa wakipita kwa mamia na kwa maelfu, na Daudi na watu wake walikuwa wakipita baadaye pamoja na Akishi.+ 3 Nao wakuu wa Wafilisti wakaanza kusema: “Hawa Waebrania+ wanataka nini?” Naye Akishi akawaambia wakuu wa Wafilisti: “Je, huyu si Daudi mtumishi wa Sauli mfalme wa Israeli, aliyekuwa pamoja nami hapa mwaka mmoja au miwili,+ nami sijapata+ndani yake jambo hata moja tangu siku ile alipotoroka kuja kwangu mpaka leo hii?” 4 Nao wakuu wa Wafilisti wakamghadhibikia; na wakuu Wafilisti wakaendelea kumwambia: “Mrudishe mtu huyo,+ mwache arudi mahali ulipompa; wala usiache ashuke pamoja nasi kwenda vitani, asije akawa mpinzani+ wetu katika vita. Na je, mtu huyu atajipatia kibali kwa bwana wake jinsi gani? Je, si kwa vichwa vya watu wetu? 5 Je, huyu si Daudi ambaye waliendelea kuitikia katika kucheza dansi, wakisema, ‘Sauli amepiga maelfu yake, na Daudi makumi ya maelfu yake’?”+
6 Basi Akishi+ akamwita Daudi na kumwambia: “Kama Yehova anavyoishi,+ wewe ni mnyoofu, na kutoka kwako na kuingia kwako+ pamoja nami katika kambi kumekuwa kwema machoni pangu;+ kwa maana sijapata ubaya ndani yako tangu siku ile ulipokuja kwangu mpaka leo hii.+ Lakini machoni pa wakuu wa muungano+ wewe si mwema. 7 Na sasa rudi, uende kwa amani, usije ukafanya jambo lolote baya machoni pa wakuu wa muungano wa Wafilisti.” 8 Hata hivyo, Daudi akamwambia Akishi: “Kwani nimefanya nini,+ nawe umepata nini ndani ya mtumishi wako tangu siku ile nilipokuja mbele yako mpaka leo hii,+ ili nisije na kupigana na adui za bwana wangu mfalme?” 9 Ndipo Akishi akajibu na kumwambia Daudi: “Najua vema kwamba umekuwa mwema machoni pangu, kama malaika wa Mungu.+ Ila wakuu wa Wafilisti ndio wamesema, ‘Asipande pamoja nasi kwenda vitani.’ 10 Na sasa ondokeni asubuhi na mapema pamoja na watumishi wa bwana wako waliokuja nawe; nanyi mwondoke asubuhi na mapema wakati kutakapokuwa kumewapambazukia. Kisha mwende zenu.”+
11 Basi Daudi akaondoka mapema, yeye na watu wake, ili waende asubuhi+ na kurudi katika nchi ya Wafilisti; nao Wafilisti wakapanda, wakaenda Yezreeli.+