Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 18:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Nao watawahukumu watu kwenye kila pindi inayofaa; na itakuwa kwamba kila kesi kubwa watakuletea wewe,+ lakini kila kesi ndogo wao wenyewe wataishughulikia wakiwa waamuzi. Kwa hiyo jirahisishie mambo, nao wataubeba mzigo pamoja nawe.+

  • Kumbukumbu la Torati 16:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Utaweka waamuzi+ na maofisa+ kwa ajili yako ndani ya malango yote ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe kulingana na makabila yako, nao watawahukumu watu kwa hukumu ya uadilifu.

  • Kumbukumbu la Torati 25:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 “Ikiwa mzozo utatokea kati ya watu,+ nao wamejitokeza kwa ajili ya hukumu,+ watawahukumu na kumtangaza mwadilifu kuwa mwadilifu na mwovu kuwa mwovu.+

  • 1 Samweli 2:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Mwanadamu akifanya dhambi juu ya mwanadamu,+ Mungu atakuwa mwamuzi wake;+ lakini mwanadamu akifanya dhambi juu ya Yehova,+ ni nani atakayetoa sala kwa ajili yake?”+ Lakini hawakuisikiliza sauti ya baba+ yao, kwa sababu sasa Yehova alitaka kuwaua.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 19:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Na kuhusu kila kesi itakayokuja kwenu ya ndugu zenu wanaokaa katika majiji yao, inayohusu kumwaga damu,+ inayohusu sheria+ na amri+ na masharti+ na maamuzi ya hukumu,+ lazima mwaonye kwamba wasimkosee Yehova ili ghadhabu+ isije juu yenu na juu ya ndugu zenu. Hivyo ndivyo mnavyopaswa kufanya ili msipate hatia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki