Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 15:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Unapaswa kumpa hata iweje,+ nao moyo wako usiwe mchoyo unapompa, maana kwa sababu hiyo Yehova Mungu wako atakubariki katika kila tendo lako na katika kila kazi unayofanya.+

  • Methali 11:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Kuna mtu anayetawanya na bado anaongezewa;+ pia kuna mtu anayewanyima wengine yaliyo sawa, lakini hilo huleta uhitaji tu.+

  • Methali 14:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Anayemdharau mwenzake anatenda dhambi,+ lakini mwenye furaha ni yule anayewaonyesha kibali wenye kuteseka.+

  • Methali 19:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova,+ na Yeye atamlipa matendo yake.+

  • Luka 6:38
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 38 Muwe na mazoea ya kuwapa watu, na watu watawapa ninyi.+ Watawamwagia katika mfuko wa nguo zenu kipimo kizuri, kilichoshindiliwa, kilichotikiswa pamoja na kufurika. Kwa maana kwa kipimo mnachopimia, watawapimia ninyi pia.”+

  • 2 Wakorintho 9:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Lakini kuhusu hili, yeye anayepanda kwa uhaba+ atavuna pia kwa uhaba; na yeye anayepanda kwa wingi+ atavuna pia kwa wingi.

  • 1 Yohana 3:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Lakini yeyote aliye na riziki ya ulimwengu huu+ naye amwone ndugu yake akiwa na uhitaji+ na bado amfungie mlango wa huruma zake nyororo,+ ni katika njia gani kumpenda Mungu hukaa ndani yake?+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki