14 Lakini sasa ufalme wako hautadumu.+ Yehova atajitafutia mtu anayekubalika kwa moyo wake;+ na Yehova atamweka kuwa kiongozi+ juu ya watu wake, kwa sababu wewe hukushika yale aliyokuamuru Yehova.”+
28 Ndipo Samweli akamwambia: “Yehova ameurarua+ utawala wa kifalme wa Israeli kutoka kwako leo, naye hakika atampa mwenzako ambaye ni bora kuliko wewe.+
13 Basi Samweli akachukua ile pembe ya mafuta,+ akamtia mafuta katikati ya ndugu zake. Na roho ya Yehova ikaanza kutenda kazi juu ya Daudi kuanzia siku hiyo na kuendelea.+ Baadaye Samweli akasimama, akaenda zake mpaka Rama.+
31 Kwa maana siku zote ambazo mwana wa Yese atakuwa hai katika nchi, wewe na ufalme wako hutasimama imara.+ Basi sasa tuma watu umlete kwangu, kwa maana amekusudiwa kufa.”+