26 Ahazia alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala, naye akatawala mwaka mmoja katika Yerusalemu.+ Na jina la mama yake lilikuwa Athalia+ mjukuu wa Omri+ mfalme wa Israeli.
6 Naye akaendelea kutembea katika njia ya wafalme wa Israeli,+ kama walivyofanya wale wa nyumba ya Ahabu; kwa maana binti ya Ahabu alikuwa amekuwa mke wake,+ naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+
10 Kwa habari ya Athalia+ mama ya Ahazia, yeye aliona kwamba mwana wake amekufa. Kwa hiyo akasimama, akauangamiza uzao wote wa kifalme wa nyumba ya Yuda.+
7 Kwa maana wana wa Athalia yule mwanamke mwovu+ walikuwa wamevunja na kuingia ndani ya nyumba ya Mungu wa kweli,+ na hata vitu vyote vitakatifu+ vya nyumba ya Yehova walikuwa wamevitolea Mabaali.”+