Yakobo
4 Vita vinatoka chanzo gani na mapigano yanatoka chanzo gani katikati yenu? Je, havitoki katika chanzo hiki,+ yaani, katika tamaa zenu za mwili zinazoendeleza pambano katika viungo vyenu?+ 2 Mnatamani, na bado hamna kitu. Mnaendelea kuua+ na kutamani+ kwa wivu, na bado hamwezi kupata. Mnaendelea kupigana+ na kufanya vita. Hamna kitu kwa sababu hamwombi. 3 Mnaomba, na bado hampokei, kwa sababu mnaomba kwa kusudi baya,+ ili mvitumie kwa tamaa zenu za mwili.+
4 Enyi wazinzi,+ je, hamjui kwamba urafiki na ulimwengu ni uadui na Mungu?+ Kwa hiyo, yeyote anayetaka kuwa rafiki+ ya ulimwengu anajifanya kuwa adui ya Mungu.+ 5 Au je, inaonekana kwenu kwamba andiko linasema hivi bila kusudi lolote: “Roho+ ambayo imefanya makao ndani yetu hutamani kuwa na mwelekeo wa kuona wivu”? 6 Hata hivyo, fadhili zisizostahiliwa ambazo yeye hutoa ni kubwa zaidi.+ Kwa hiyo, hilo linasema: “Mungu huwapinga wenye majivuno,+ lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.”+
7 Basi, jitiisheni+ kwa Mungu; lakini mpingeni Ibilisi,+ naye atawakimbia ninyi.+ 8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.+ Safisheni mikono yenu, ninyi watenda-dhambi,+ na takaseni mioyo yenu,+ ninyi wenye kusitasita.+ 9 Iweni na taabu na kuomboleza na kulia.+ Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa maombolezo, na shangwe yenu kuwa huzuni.+ 10 Jinyenyekezeni machoni pa Yehova,+ naye atawainua ninyi.+
11 Mwache kusemana wenyewe, akina ndugu.+ Yeye anayesema vibaya juu ya ndugu au anayemhukumu+ ndugu yake husema vibaya juu ya sheria na kuihukumu sheria. Na ikiwa unaihukumu sheria, basi wewe si mtendaji wa sheria, bali ni mwamuzi.+ 12 Kuna mmoja ambaye ni mpaji-sheria na mwamuzi,+ ambaye anaweza kuokoa na kuangamiza.+ Lakini wewe ni nani ili uwe ukimhukumu jirani yako?+
13 Haya, basi, ninyi ambao husema: “Leo au kesho tutasafiri kwenda jiji fulani nasi tutakaa mwaka mmoja huko, tutafanya biashara na kupata faida,”+ 14 ingawa hamjui uzima wenu utakuwa namna gani kesho.+ Kwa maana ninyi ni ukungu unaotokea kwa muda kidogo na kisha kutoweka.+ 15 Badala yake, mnapaswa kusema: “Yehova akipenda,+ tutaishi na pia kufanya hili au lile.”+ 16 Lakini sasa mnajivunia kujigamba kwenu kwa kujidai.+ Majivuno yote ya namna hiyo ni maovu. 17 Kwa hiyo, ikiwa mtu anajua jinsi ya kufanya yaliyo sawa na bado hayafanyi,+ hiyo ni dhambi+ kwake.