Isaya
62 Sitanyamaza kwa ajili ya Sayuni,+
Nami sitatulia kwa ajili ya Yerusalemu
Mpaka uadilifu wake ung’ae kama mwangaza mkali+
Na wokovu wake uwake kama mwenge.+
Nawe utaitwa kwa jina jipya,+
Ambalo kinywa cha Yehova mwenyewe kitalichagua.
3 Utakuwa taji la urembo mkononi mwa Yehova,
Kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako.
Lakini utaitwa Furaha Yangu Imo Ndani Yake,+
Na nchi yako itaitwa Aliyeolewa.
Kwa maana Yehova atafurahishwa nawe,
Na nchi yako itakuwa kama aliyeolewa.
5 Kwa maana kama kijana wa kiume anavyomwoa msichana bikira,
Ndivyo wana wako watakavyokuoa.
Kama bwana harusi anavyomfurahia bibi harusi
Ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia.+
6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu.
Hawapaswi kukaa kimya daima, mchana kutwa na usiku kucha.
Ninyi mnaomtaja Yehova,
Msipumzike,
7 Na msiache kamwe apumzike mpaka aliimarishe kabisa Yerusalemu,
Naam, mpaka alifanye kuwa sifa ya dunia.”+
8 Yehova ameapa kiapo kwa mkono wake wa kuume, kwa mkono wake wenye nguvu:
“Sitawapa tena maadui wako nafaka yako iwe chakula chao,
Wala wageni hawatakunywa divai yako mpya, ambayo umetaabika kuipata.+
9 Lakini wale wanaoikusanya wataila nao watamsifu Yehova;
Na wale wanaoikusanya watainywa katika nyua zangu takatifu.”+
10 Piteni humo, piteni katika malango.
Watayarishieni watu njia.+
Tengenezeni, tengenezeni barabara kuu.
Ondoeni mawe juu yake.+
Inueni ishara* kwa ajili ya watu.+
11 Tazama! Yehova ametangaza mpaka kwenye miisho ya dunia:
“Mwambieni binti ya Sayuni,
‘Tazama! Wokovu wako unakuja.+
Tazama! Anakuja na thawabu yake,
Na malipo anayotoa yako mbele zake.’”+