Mikutano Ya Utumishi Kwa Februari
Juma Linaloanza Februari 1
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma ya Ufalme Yetu. Wakumbushe wote watoe ripoti zao za utumishi za Januari.
Dak. 17: “Toa Kitabu Furaha ya Familia kwa Watu wa Kila Umri.” Mzee azungumzia makala pamoja na wahubiri wawili au watatu wenye ustadi. Kazia mradi wa kusaidia wengine watambue kwamba siri ya furaha ya familia hupatikana kwa kufuata shauri la Biblia. (Ona Furaha ya Familia, ukurasa wa 9-12.) Toa wonyesho wa utoaji mmoja uliodokezwa. Onyesha jinsi ya kupanga ziara ya kurudia.
Dak. 18: “‘Vaeni Utu Mpya.’” Hotuba, ikichanganua Waefeso 4:20-24. (Ona Mnara wa Mlinzi, Machi 1, 1993, ukurasa wa 14-18, fungu la 4-17.) Eleza jinsi tunavyovua utu wa zamani na kuvaa ule mpya.
Wimbo 4 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 8
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: “Tulinufaika na Mikusanyiko ya ‘Njia ya Mungu ya Maisha.’” Maswali na majibu. Onyesha broshua mpya na kitabu kipya, na ueleze njia ambazo twaweza kuvitumia vizuri.
Dak. 20: “Muumba Wetu Mtukufu Hutujali!” Maswali na majibu. Eleza jinsi kitabu Muumba kinavyoweza kutumiwa kusaidia wale walio na shaka au wanaokana kuwapo kwa Mungu. Ijapokuwa kitabu hicho si cha kuongoza mafunzo ya Biblia, chaweza kuwa chombo chenye matokeo katika kuchochea watu wachunguze yale yote ambayo Biblia husema. (Ona kitabu Muumba, ukurasa wa 189-191.) Waalike wahubiri washiriki kutoa maelezo yao wenyewe kuhusu kichapo hiki na kusimulia mambo yoyote yaliyoonwa ambayo wamekuwa nayo walipowaangushia wengine kitabu hicho.
Wimbo 173 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 18: Twanufaikaje kwa Kujiandikisha Katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakiongozwa na mwangalizi wa shule. Mazoezi katika kusema hadharani silo kusudi pekee la shule. Kuna njia nyingine ambazo katika hizo twaweza kunufaika moja kwa moja. (Ona kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 12-13.) Twajifunza jinsi ya kuwasiliana vizuri zaidi na watu wengine. Twafundishwa kusema waziwazi, kutua, na kujitumaini. Tunakuwa wenye ustadi katika kujibu maswali yanayohusu itikadi zetu na kueleza maamuzi yetu yenye kutegemea Biblia. Ujuzi wetu kuhusu Biblia huongezeka, ukitusaidia tuwe wenye matokeo zaidi katika kutolea wengine ushahidi. Twajifunza kutambua makosa yetu na kukubali shauri, ikitokeza kushughulika na wengine kwa amani. Mazoezi ya jumla ambayo shule huandaa hutusaidia tudumu tukiwa na “sifa za ustahili wa kutosha” tukiwa wahudumu wa Mungu.—2 Kor. 3:5, 6.
Dak. 17: “Jinsi Ambavyo Washiriki wa Familia Hushirikiana Kikamili—Katika Funzo la Biblia.” Mazungumzo ya kikundi cha familia. Wanachanganua jinsi wanavyoweza kutumia madokezo yanayohusu usomaji wa Biblia na funzo la familia kama yapatikanavyo katika Mnara wa Mlinzi, Mei 15, 1996, ukurasa wa 14-15, na Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15, 1992, ukurasa wa 16-17.
Wimbo 57 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Kwa Nini Uweke Rekodi ya Wasiokuwepo Nyumbani?” Zungumza na wahubiri wawili au watatu juu ya makala iliyo katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei 1995. Toa wonyesho wa jinsi mhubiri mwenye uzoefu anavyomsaidia mhubiri mpya aandike maandishi yake ya Wasiokuwepo Nyumbani.
Dak. 20: Jinsi ya Kupata Shangwe Katika Kufanya Wanafunzi. Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1996, ukurasa wa 19-22.
Wimbo 91 na sala ya kumalizia.