Hosea
10 “Israeli ni mzabibu unaoharibika.+ Yeye huendelea kutokeza matunda kwa ajili yake mwenyewe.+ Naye amezidisha madhabahu zake kulingana na wingi wa matunda yake.+ Wao huweka nguzo nzuri+ kulingana na wema wa nchi yake. 2 Moyo wao umekuwa na unafiki;+ sasa watapatikana na hatia.
“Kuna yule atakayevunja madhabahu zao; atapora nguzo zao.+ 3 Kwa maana sasa watasema, ‘Hatuna mfalme yeyote,+ kwa kuwa hatukumwogopa Yehova. Naye mfalme atatufanyia nini?’
4 “Wao husema maneno, wakila viapo vya uwongo,+ wakifanya agano;+ na hukumu imechipuka kama mmea wenye sumu katika mitaro ya shamba.+ 5 Wakaaji wa Samaria wataogopa kwa sababu ya sanamu ya ndama ya Beth-aveni;+ kwa maana watu wake wataiombolezea, na vilevile makuhani wake wa miungu ya kigeni waliokuwa wakishangilia juu yake, kwa sababu ya utukufu wake, kwa maana itakuwa imeenda uhamishoni mbali nayo.+ 6 Nayo itachukuliwa Ashuru na mtu fulani iwe zawadi kwa mfalme mkuu.+ Efraimu naye atapata aibu,+ na Israeli atalionea aibu shauri lake.+ 7 Samaria na mfalme wake hakika watanyamazishwa,+ kama tawi lililokatwa juu ya uso wa maji. 8 Na mahali pa juu pa Beth-aveni,+ dhambi ya Israeli,+ pataangamizwa. Miiba na mibaruti+ itakuja juu ya madhabahu zao.+ Na hakika watu wataiambia milima, ‘Tufunikeni!’ na vilima, ‘Tuangukieni!’+
9 “Umetenda dhambi+ kuanzia siku za Gibea,+ Ee Israeli. Huko walisimama tuli. Vita juu ya wana wenye kukosa uadilifu katika Gibea havikupata kuwafikia.+ 10 Wakati nitakapopenda nitawatia nidhamu pia.+ Na vikundi vya watu vitakusanyika juu yao watakapofungwa pamoja na makosa yao mawili.+
11 “Na Efraimu alikuwa ndama-jike aliyezoezwa, anayependa kupura;+ nami mwenyewe nikapita juu ya shingo yake yenye kupendeza. Nafanya mtu fulani ampande Efraimu.+ Yuda hulima;+ Yakobo humlimia.+ 12 Mjipandie mbegu kwa uadilifu;+ mvune kulingana na fadhili zenye upendo.+ Mjilimie udongo unaofaa kwa kilimo,+ kukiwa kungali na wakati wa kumtafuta Yehova mpaka atakapokuja+ na kuwatolea ninyi mafundisho kwa uadilifu.+
13 “Ninyi mmelima uovu.+ Nanyi mmevuna ukosefu wa uadilifu.+ Mmekula matunda ya udanganyifu,+ kwa maana mmetegemea njia yenu,+ katika wingi wa watu wenu wenye nguvu.+ 14 Na fujo imetokea kati ya watu wako,+ na majiji yako yenye ngome yataporwa yote,+ kama vile Shalmani alivyopora nyumba ya Arbeli, katika siku ya pigano ambapo mama mmoja alivunjwa vipande-vipande kando ya wanawe.+ 15 Mtu fulani atawafanyia vivyo hivyo, Ee Betheli, kwa sababu ya ubaya wenu mwingi.+ Hakika mfalme wa Israeli atanyamazishwa+ wakati wa mapambazuko.”