Waefeso
2 Zaidi ya hilo, ninyi ndio ambao Mungu alifanya kuwa hai ingawa mlikuwa wafu katika makosa na dhambi zenu,+ 2 ambazo wakati fulani mlitembea ndani yake kulingana na mfumo wa mambo+ wa ulimwengu huu, kulingana na mtawala+ wa mamlaka ya hewa, roho+ ambayo sasa hutenda katika wana wa kutotii.+ 3 Ndiyo, wakati fulani sisi sote tulijiendesha katikati yao kupatana na tamaa za mwili wetu,+ tukifanya mambo yanayopendwa na mwili+ na fikira, nasi kiasili tulikuwa watoto wa ghadhabu+ sawa na wale wengine. 4 Lakini Mungu, aliye tajiri katika rehema,+ kwa upendo wake mkubwa aliotupenda nao,+ 5 alitufanya hai pamoja na Kristo, tulipokuwa wafu katika makosa+—kwa fadhili zisizostahiliwa ninyi mmeokolewa+— 6 naye alituinua+ pamoja na kutuketisha pamoja katika mahali pa kimbingu+ katika muungano na Kristo Yesu, 7 ili katika mifumo ya mambo inayokuja+ uonyeshwe utajiri+ mwingi zaidi wa fadhili zake zisizostahiliwa katika neema yake kutuelekea sisi katika muungano+ na Kristo Yesu.
8 Kwa fadhili hizi zisizostahiliwa, kwa kweli, ninyi mmeokolewa kupitia imani;+ na hiyo si kutokana na ninyi,+ ni zawadi ya Mungu.+ 9 Hapana, si kutokana na matendo,+ ili mtu yeyote asiwe na sababu ya kujisifu.+ 10 Kwa maana sisi ni matokeo ya kazi yake+ na tuliumbwa+ katika muungano+ na Kristo Yesu kwa ajili ya matendo mema,+ ambayo Mungu alitutayarishia kimbele+ ili tutembee katika hayo.
11 Kwa hiyo endeleeni kukumbuka akilini kwamba hapo zamani mlikuwa watu wa mataifa kwa habari ya mwili;+ “kutotahiriwa” ndivyo mlivyoitwa na kile kinachoitwa “kutahiriwa” ambacho kimefanywa mwilini kwa mikono+— 12 kwamba wakati huo mlikuwa bila Kristo,+ mlikuwa mmetengwa mbali+ na taifa la Israeli nanyi mlikuwa wageni kwa maagano ya ahadi,+ wala hamkuwa na tumaini+ na mlikuwa bila Mungu katika ulimwengu.+ 13 Lakini sasa katika muungano na Kristo Yesu ninyi ambao wakati mmoja mlikuwa mbali sana mmekuja kuwa karibu kupitia damu+ ya Kristo. 14 Kwa maana yeye ni amani yetu,+ yeye aliyefanya vile vikundi viwili+ kuwa kimoja+ na kuuharibu ukuta+ wa katikati uliowatenganisha.+ 15 Kwa njia ya mwili wake+ aliufuta uadui,+ ile Sheria ya amri zilizofanyizwa kwa maagizo,+ ili aumbe vile vikundi viwili vya watu+ katika muungano na yeye mwenyewe viwe mtu mmoja mpya+ na kufanya amani; 16 na ili avipatanishe+ kwa ukamili hivyo vikundi viwili vya watu+ katika mwili mmoja kwa Mungu kupitia mti wa mateso,+ kwa sababu alikuwa ameua ule uadui+ kwa njia ya yeye mwenyewe. 17 Naye alikuja na kuwatangazia ninyi habari njema ya amani,+ wale waliokuwa mbali sana, na amani kwa wale waliokuwa karibu,+ 18 kwa sababu kupitia yeye, sisi, vikundi vyote viwili vya watu,+ tunaweza kumkaribia+ Baba kwa roho moja.+
19 Hakika, basi, ninyi si wageni+ tena na wakaaji wageni,+ bali ninyi ni raia wenzi+ wa watakatifu+ na ni washiriki wa nyumba+ ya Mungu, 20 nanyi mmejengwa juu ya msingi+ wa mitume+ na manabii,+ naye Kristo Yesu mwenyewe akiwa ndiye jiwe la msingi la pembeni.+ 21 Katika muungano na yeye, jengo lote likiunganishwa pamoja+ kwa upatano, linakua liwe hekalu takatifu kwa ajili ya Yehova.+ 22 Katika muungano+ na yeye, ninyi pia mnajengwa pamoja muwe mahali pa Mungu pa kukaa kwa njia ya roho.+