Wafilipi
Kwa Wafilipi
1 Paulo na Timotheo, watumwa+ wa Kristo Yesu, kwa watakatifu wote katika muungano na Kristo Yesu walio katika Filipi,+ pamoja na waangalizi na watumishi wa huduma:+
2 Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.+
3 Namshukuru Mungu wangu sikuzote kila mara ninapowakumbuka ninyi+ 4 katika dua zangu zote kwa ajili yenu nyote,+ ninapoendelea kutoa dua yangu kwa shangwe, 5 kwa sababu ya mchango+ ambao mmeutoa kwa ajili ya habari njema tangu siku ya kwanza mpaka sasa. 6 Kwa maana nina uhakika juu ya jambo hili, kwamba yeye aliyeanza kazi njema katika ninyi ataiendeleza mpaka aikamilishe+ kufikia siku+ ya Yesu Kristo. 7 Ni sawa kabisa kwangu kufikiri hili kuwahusu ninyi nyote, kwa sababu ya mimi kuwa nanyi katika moyo wangu,+ ninyi nyote mkiwa washiriki+ pamoja nami katika fadhili zisizostahiliwa, katika vifungo vyangu vya gereza+ na katika kutetea+ na kuithibitisha kisheria+ habari njema.
8 Kwa maana Mungu ni shahidi wangu kuhusu jinsi ninavyowatamani sana ninyi nyote kwa namna ya upendo mwororo+ kama alio nao Kristo Yesu. 9 Na hili ndilo ninaloendelea kusali, kwamba upendo wenu uwe mwingi+ hata zaidi na zaidi pamoja na ujuzi sahihi+ na utambuzi kamili;+ 10 kwamba mhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi,+ ili muwe bila kasoro+ na msiwe mkiwakwaza+ wengine mpaka siku ya Kristo, 11 na mjazwe matunda ya uadilifu,+ ambayo ni kupitia Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa kwa Mungu.+
12 Basi nataka mjue, akina ndugu, kwamba mambo yangu yamegeuka na kuwa yenye kuendeleza mbele habari njema+ badala ya kuwa kinyume, 13 hivi kwamba vifungo vyangu+ vimejulikana kwa watu wote+ kwa kushirikiana na Kristo kati ya Walinzi wote wa Mfalme na wale wengine wote;+ 14 na walio wengi kati ya akina ndugu katika Bwana, wakihisi uhakika kwa sababu ya vifungo vyangu vya gereza, wanaonyesha uhodari hata zaidi kulisema neno la Mungu bila woga.+
15 Ni kweli, wengine wanamhubiri Kristo kwa wivu na kushindana,+ lakini wengine pia kwa nia njema.+ 16 Hao wa mwisho wanamtangaza Kristo kutokana na upendo, kwa maana wanajua kwamba mimi nimewekwa hapa kwa ajili ya kutetea+ habari njema; 17 lakini wale wa kwanza hufanya hivyo kutokana na ugomvi,+ si kwa kusudi safi, kwa maana wanataka kuchochea dhiki+ juu yangu katika vifungo vyangu vya gereza. 18 Nini basi? Si kitu, isipokuwa tu kwa kila njia, kama ni kwa unafiki+ au ni kwa kweli, Kristo anatangazwa,+ nami nashangilia katika jambo hilo. Kwa kweli, nitaendelea pia kushangilia, 19 kwa maana najua hilo litatokeza wokovu wangu kupitia dua+ yenu na gawio la roho ya Yesu Kristo,+ 20 kwa kupatana na tarajio langu lenye hamu+ na tumaini+ kwamba sitaona aibu+ kwa njia yoyote, bali kwamba katika uhuru wote wa kusema,+ Kristo, kama sikuzote hapo mwanzoni, atatukuzwa hivyo sasa kwa njia ya mwili wangu,+ iwe ni kupitia uzima au ni kupitia kifo.+
21 Kwa maana kwa habari yangu kuishi ni Kristo,+ na kufa+ ni faida. 22 Basi ikiwa ni kuendelea kuishi katika mwili, hilo ni tunda la kazi yangu+—na bado jambo la kuchagua silifanyi lijulikane. 23 Niko chini ya mkazo kutokana na mambo haya mawili;+ lakini kile ninachotamani ni kule kufunguliwa na kule kuwa pamoja na Kristo,+ kwa maana hili, kwa hakika, ni bora zaidi.+ 24 Hata hivyo, mimi kubaki katika mwili ni lazima zaidi kwa sababu yenu.+ 25 Kwa hiyo, nikiwa na uhakika juu ya hili, najua nitabaki+ nami nitakaa pamoja na ninyi nyote kwa ajili ya ninyi kuendelea mbele+ na shangwe ya imani yenu, 26 ili furaha yenu ifurike katika Kristo Yesu kwa sababu yangu kupitia kuwapo kwangu tena pamoja nanyi.
27 Ila tu jiendesheni kwa namna inayostahili+ habari njema juu ya Kristo, ili, kama nitakuja na kuwaona ninyi au kama sitakuwapo, nisikie juu ya mambo yanayowahusu ninyi, kwamba mnasimama imara katika roho moja, kwa nafsi moja+ mkikazana pamoja kwa ajili ya imani ya habari njema, 28 nanyi msiwaogope hata kidogo wapinzani+ wenu. Jambo hili ni uthibitisho wa uharibifu kwao, lakini wa wokovu kwenu;+ na ishara hii inatokana na Mungu, 29 kwa sababu ninyi mlipewa pendeleo kwa ajili ya Kristo, si muwe tu na imani+ katika yeye, bali pia mteseke+ kwa ajili yake. 30 Kwa maana ninyi mna pambano lilelile kama mlivyoona kunihusu mimi+ na kama mnavyosikia sasa kunihusu mimi.+