Yoshua
12 Basi hawa ndio wafalme wa nchi ambao wana wa Israeli waliwashinda, na kuimiliki nchi yao ng’ambo ya Yordani upande wa mapambazuko ya jua,+ kutoka bonde la mto la Arnoni+ hadi Mlima Hermoni+ na Araba+ yote upande wa mashariki: 2 Sihoni+ mfalme wa Waamori, aliyekaa katika Heshboni,+ akitawala kutoka Aroeri,+ lililokuwa kwenye ukingo wa bonde la mto la Arnoni,+ na katikati ya bonde la mto, na nusu ya Gileadi hadi bonde la mto la Yaboki,+ mpaka wa wana wa Amoni, 3 na Araba+ hadi bahari ya Kinerethi+ kuelekea mashariki hadi bahari ya Araba, yaani, Bahari ya Chumvi,+ upande wa mashariki kuelekea Beth-yeshimothi,+ na kuelekea kusini chini ya miteremko ya Pisga.+
4 Na eneo la Ogu+ mfalme wa Bashani, lile lililobaki la Warefaimu,+ waliokaa katika Ashtarothi+ na Edrei,+ 5 na waliotawala katika Mlima Hermoni+ na katika Saleka na katika Bashani+ yote, hadi mpaka wa Wageshuri+ na Wamaakathi,+ na nusu ya Gileadi, hadi katika eneo la Sihoni+ mfalme wa Heshboni.+
6 Musa mtumishi wa Yehova na wana wa Israeli ndio waliowashinda,+ kisha Musa mtumishi wa Yehova akawapa Warubeni+ na Wagadi+ na nusu ya kabila la Manase+ iwe urithi wao.
7 Na hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na wana wa Israeli waliwashinda ng’ambo ya Yordani kuelekea magharibi, kuanzia Baal-gadi+ katika nchi tambarare ya bondeni ya Lebanoni+ hadi Mlima Halaki,+ unaopanda hadi Seiri,+ kisha Yoshua akawapa makabila ya Israeli iwe urithi wao kulingana na mafungu yao,+ 8 katika eneo lenye milima na katika Shefela na katika Araba na kwenye miteremko na katika nyika na katika Negebu+—Wahiti, Waamori+ na Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi:+
9 Mfalme wa Yeriko,+ mmoja; mfalme wa Ai,+ jiji lililokuwa kando ya Betheli, mmoja;
10 mfalme wa Yerusalemu,+ mmoja; mfalme wa Hebroni,+ mmoja;
11 mfalme wa Yarmuthi,+ mmoja; mfalme wa Lakishi,+ mmoja;
12 mfalme wa Egloni,+ mmoja; mfalme wa Gezeri,+ mmoja;
13 mfalme wa Debiri,+ mmoja; mfalme wa Gederi, mmoja;
14 mfalme wa Horma, mmoja; mfalme wa Aradi, mmoja;
15 mfalme wa Libna,+ mmoja; mfalme wa Adulamu, mmoja;
16 mfalme wa Makeda,+ mmoja; mfalme wa Betheli,+ mmoja;
17 mfalme wa Tapua, mmoja; mfalme wa Heferi,+ mmoja;
18 mfalme wa Afeki, mmoja; mfalme wa Lasharoni, mmoja;
19 mfalme wa Madoni,+ mmoja; mfalme wa Hasori,+ mmoja;
20 mfalme wa Shimron-meroni, mmoja; mfalme wa Akshafi,+ mmoja;
21 mfalme wa Taanaki, mmoja; mfalme wa Megido,+ mmoja;
22 mfalme wa Kedeshi, mmoja; mfalme wa Yokneamu+ katika Karmeli, mmoja;
23 mfalme wa Dori katika safu ya milima ya Dori,+ mmoja; mfalme wa Goiimu katika Gilgali, mmoja;