11 “Wewe kwa upande wako shika ninalokuamuru leo.+ Tazama, ninawafukuza toka mbele yako Waamori na Wakanaani na Wahiti na Waperizi na Wahivi na Wayebusi.+
16 Nawe utawaangamiza watu wote ambao Yehova Mungu wako anawatia mkononi mwako.+ Jicho lako lisiwasikitikie;+ wala usiitumikie miungu yao,+ kwa sababu jambo hilo litakuwa mtego kwako.+
5 Hutaimiliki nchi yao kwa sababu ya uadilifu+ wako wala kwa sababu ya unyoofu wa moyo wako;+ kwa kweli, Yehova anayafukuzia mbali mataifa haya kutoka mbele yako+ kwa sababu ya uovu wao, na ili kulitimiza neno ambalo Yehova aliwaapia mababu zako, Abrahamu,+ Isaka+ na Yakobo.+
7 Je, wewe mwenyewe, Ee Mungu wetu,+ hukuwafukuza wakaaji wa nchi hii kutoka mbele ya watu wako Israeli,+ kisha ukaikabidhi+ kwa uzao wa Abrahamu, mpendwa wako,+ mpaka wakati usio na kipimo?