Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 32:39
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 39 Oneni sasa kwamba mimi—mimi ndiye+

      Na hakuna miungu pamoja nami.+

      Mimi huua, nami hufanya hai.+

      Nimejeruhi vikali,+ na mimi—mimi nitaponya,+

      Na hakuna anayenyakua kutoka mkononi mwangu.+

  • 1 Samweli 2:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Yehova ni Mwenye Kuua na Mwenye Kuhifadhi uhai,+

      Ni Mwenye Kushusha mpaka katika Kaburi,*+ na Yeye huinua.+

  • 2 Wafalme 4:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Mwishowe akaenda juu, akajilaza juu ya yule mtoto,+ akakitia kinywa chake juu ya kinywa chake, na macho yake juu ya macho yake, na mikono yake juu ya mikono yake, akaendelea kuinama juu yake, na hatua kwa hatua mwili wa mtoto ukawa na joto.

  • 2 Wafalme 13:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Na ikawa kwamba walipokuwa wakimzika mtu, tazama, wakaona kikundi cha waporaji. Wakamtupa mara moja yule mtu ndani ya kaburi la Elisha, wakaenda zao. Mtu yule alipoigusa mifupa ya Elisha, akawa hai+ mara moja na kusimama kwa miguu+ yake.

  • Luka 7:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Na huyo mfu akaketi na kuanza kusema, naye akamkabidhi kwa mama yake.+

  • Luka 8:55
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 55 Na roho+ yake ikarudi, naye akainuka+ mara moja, na Yesu akaagiza apewe kitu ale.+

  • Yohana 5:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Msistaajabie jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho+ wataisikia sauti yake

  • Yohana 11:44
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 44 Huyo mtu aliyekuwa mfu akatoka miguu na mikono yake ikiwa imefungwa vitambaa,+ na uso wake ulikuwa umefungwa-fungwa kwa kitambaa. Yesu akawaambia: “Mfungueni, mmwache aende.”

  • Matendo 9:41
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 41 Petro akampa mkono wake, akamwinua,+ naye akawaita watakatifu na wajane na akamweka mbele yao akiwa hai.+

  • Matendo 20:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Lakini Paulo akashuka kutoka ghorofani, akajitupa juu yake+ akamkumbatia na kusema: “Acheni kufanya kelele, kwa maana nafsi yake imo ndani yake.”+

  • Waroma 14:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Kwa maana kwa kusudi hili Kristo alikufa na kuwa hai tena,+ ili awe Bwana juu ya waliokufa+ na walio hai+ pia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki