16 “Samaria atahesabiwa kuwa na hatia,+ kwa maana kwa kweli yeye amemwasi Mungu wake.+ Wataanguka kwa upanga.+ Watoto wao wenyewe watavunjwa vipande-vipande,+ na wanawake wao wenye mimba watapasuliwa.”+
11 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kuna adui kuzunguka nchi,+ naye atazishusha nguvu zako zikutoke, na minara ya makao yako itaporwa.’+
6 Nami nitalifanya Samaria kuwa rundo la mabomoko ya shambani,+ mahali pa kupanda mizabibu; nami nitamwaga mawe yake katika bonde, na misingi yake nitaifunua.+
16 Na sheria za Omri+ na kazi yote ya nyumba ya Ahabu zinafuatwa,+ nanyi mnatembea katika mashauri yao;+ ili mimi niwafanye ninyi kuwa kitu cha kushangaza na wakaaji wake kuwa kitu cha kupigiwa mluzi kwa mshangao;+ nanyi mtachukua shutuma ya vikundi vya watu.”+