Mika
6 Tafadhali, sikieni jambo ambalo Yehova anasema.+ Simameni, endesheni kesi na milima, vilima na visikie sauti yenu.+ 2 Sikieni, enyi milima, sikieni kesi ya Yehova, pia ninyi vyombo vya kudumu, ninyi misingi ya dunia;+ kwa maana Yehova ana kesi na watu wake, naye atahojiana na Israeli:+
3 “Enyi watu wangu,+ nimewafanya nini? Nami nimewachosha kwa njia gani?+ Toeni ushuhuda juu yangu.+ 4 Kwa maana niliwaleta ninyi kutoka nchi ya Misri,+ nami niliwakomboa kutoka nyumba ya watumwa;+ nami nikawatuma Musa, Haruni na Miriamu+ mbele yenu. 5 Tafadhali, enyi watu wangu, kumbukeni+ lile ambalo Balaki mfalme wa Moabu alishauri,+ na lile ambalo Balaamu mwana wa Beori alimjibu.+ Ilikuwa kutoka Shitimu+ mpaka Gilgali,+ kusudi matendo ya uadilifu ya Yehova yajulikane.”+
6 Nitamkaribia Yehova na nini?+ Nitajiinamisha na nini kwa Mungu aliye juu?+ Je, nimkaribie na matoleo mazima ya kuteketezwa,+ na ndama wenye umri wa mwaka mmoja? 7 Je, Yehova atapendezwa na maelfu ya kondoo-dume, na makumi ya maelfu ya mito ya mafuta?+ Je, nimtoe mwanangu mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya maasi yangu, uzao wa tumbo langu kwa ajili ya dhambi ya nafsi yangu?+ 8 Ee mtu wa udongo, yeye amekuambia yaliyo mema.+ Na Yehova anataka nini kutoka kwako ila kutenda haki+ na kupenda fadhili+ na kuwa na kiasi+ katika kutembea na Mungu wako?+
9 Sauti ya Yehova inaliita jiji,+ naye mtu mwenye hekima inayotumika ataliogopa jina lako.+ Ninyi isikieni fimbo na yeye aliyeiweka.+ 10 Je, bado kuna hazina za uovu katika nyumba ya mwovu,+ na kipimo cha efa kilichobanwa ambacho kimeshutumiwa? 11 Je, naweza kuwa safi kiadili nikiwa na mizani ya uovu pamoja na mfuko wa mawe ya mizani ya udanganyifu?+ 12 Kwa maana watu wake mwenyewe walio matajiri wamejaa jeuri, na wakaaji wake mwenyewe wamesema uwongo,+ na ulimi wao una udanganyifu kinywani mwao.+
13 “Nami pia, nitakufanya mgonjwa kwa kukupiga;+ utafanywa ukiwa, kwa sababu ya dhambi zako.+ 14 Nawe utakula wala hutashiba, nawe utakuwa na njaa.+ Nawe utaondoa vitu, lakini hutavichukua na kuvipeleka salama; na chochote ambacho utachukua na kukipeleka salama, nitakitoa kwa upanga.+ 15 Nawe utapanda mbegu, bali hutavuna. Nawe utakanyaga zeituni, bali hutajipaka mafuta; pia divai tamu, bali hutakunywa divai.+ 16 Na sheria za Omri+ na kazi yote ya nyumba ya Ahabu zinafuatwa,+ nanyi mnatembea katika mashauri yao;+ ili mimi niwafanye ninyi kuwa kitu cha kushangaza na wakaaji wake kuwa kitu cha kupigiwa mluzi kwa mshangao;+ nanyi mtachukua shutuma ya vikundi vya watu.”+