Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 26:33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Nami nitawatawanya ninyi katikati ya mataifa,+ nami nitauchomoa upanga nyuma yenu;+ nayo nchi yenu itakuwa ukiwa,+ na majiji yenu yatakuwa bomoko lenye ukiwa.

  • Kumbukumbu la Torati 4:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 leo nachukua mbingu na dunia ili ziwe mashahidi dhidi yenu,+ ya kwamba hakika mtaangamia haraka kutoka katika nchi ambayo mnavuka Yordani ili mwimiliki. Hamtarefusha siku zenu juu yake, kwa sababu hakika mtaangamizwa.+

  • Kumbukumbu la Torati 28:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Yehova atakufanya wewe na mfalme wako ambaye umemweka juu yako mpige mwendo+ mpaka taifa ambalo hukujua, wala wewe wala mababu zako; na huko utalazimika kuitumikia miungu mingine, ya miti na ya mawe.+

  • Kumbukumbu la Torati 28:64
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 64 “Na Yehova atakutawanya katikati ya vikundi vyote vya watu kutoka mwisho mmoja wa dunia mpaka mwisho mwingine wa dunia,+ na huko utalazimika kuitumikia miungu mingine ambayo hukuijua, wala wewe wala mababu zako, miti na mawe.+

  • 2 Wafalme 23:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Lakini Yehova akasema: “Nitaondoa Yuda+ pia mbele za macho yangu,+ kama nilivyoondoa Israeli;+ nami nitalikataa jiji hili ambalo nimechagua, naam, Yerusalemu, na nyumba ambayo nimesema hivi kuihusu, ‘Jina langu litaendelea kuwa humo.’”+

  • Yeremia 24:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 mimi pia nitawatoa kwa ajili ya kutetemesha, kwa ajili ya msiba, katika falme zote za dunia,+ kwa ajili ya shutuma na kwa ajili ya neno la kimethali, kwa ajili ya suto+ na kwa ajili ya laana,+ katika mahali pote nitakapowatawanya.+

  • Yeremia 25:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Na nchi hii yote itakuwa mahali palipoharibiwa, kitu cha kushangaza, na mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babiloni miaka 70.”’+

  • Ezekieli 12:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 ‘ “Kwa maana mimi mwenyewe, Yehova, nitasema neno nitakalosema, nalo litafanywa.+ Hakutakuwa na kucheleweshwa tena,+ kwa maana katika siku zenu,+ Ee nyumba yenye kuasi, nitasema neno na kulifanya hakika,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’ ”

  • Ezekieli 24:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.+ Lazima ije,+ nami nitatenda. Sitapuuza,+ wala sitasikitika + wala kujuta.+ Kulingana na njia zako na kulingana na matendo yako hakika watakuhukumu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki