Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 4:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Nanyi mtazishika na kuzifanya, kwa sababu hiyo ni hekima+ kwenu na uelewaji+ kwenu mbele ya macho ya vikundi vya watu watakaosikia juu ya masharti yote haya, nao watasema, ‘Taifa hili kubwa bila shaka ni watu wenye hekima na wenye uelewaji.’+

  • Ayubu 23:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Siondoki katika amri ya midomo yake.+

      Nimeyachukua kuwa hazina maneno ya kinywa chake+ kuliko yale niliyoamriwa.

  • Zaburi 19:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Sheria+ ya Yehova ni kamilifu,+ huirudisha nafsi.+

      Kikumbusho+ cha Yehova ni chenye kutegemeka,+ humfanya asiye na uzoefu awe na hekima.+

  • Zaburi 107:43
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 43 Ni nani mwenye hekima? Atayashika mambo

      hayo+

      Na kukaza fikira zake kwa matendo ya Yehova ya fadhili zenye upendo.+

  • Zaburi 119:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  34 Unifanye nielewe, ili nipate kuishika sheria yako+

      Nami nipate kuishika kwa moyo wote.+

  • Zaburi 119:100
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 100 Najiendesha kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee,+

      Kwa sababu nimeyashika maagizo yako.+

  • 2 Timotheo 3:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 na kwamba tangu utoto mchanga+ umeyajua maandishi matakatifu, ambayo yanaweza kukufanya uwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu+ kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki