Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 32:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Kwa maana Yehova atawahukumu watu wake+

      Naye atajuta juu ya watumishi wake,+

      Kwa sababu ataona kwamba tegemeo limetoweka

      Na aliyeko tu ni mtu asiye na uwezo na asiye na thamani.

  • Zaburi 103:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kama vile baba anavyowaonyesha wanawe rehema,+

      Ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa.+

  • Isaya 60:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Na wageni kwa kweli watazijenga kuta zako,+ na wafalme wao wenyewe watakuhudumia;+ kwa maana nitakuwa nimekwisha kukupiga katika ghadhabu yangu,+ lakini katika nia yangu njema hakika nitakuwa nimekuonyesha rehema.+

  • Maombolezo 3:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Ni kutokana na matendo ya fadhili zenye upendo+ za Yehova kwamba hatujaisha,+ kwa maana hakika rehema zake hazitakoma.+

  • Hosea 11:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 “Nawezaje kukuacha, Ee Efraimu?+ Nawezaje kukutoa, Ee Israeli?+ Nawezaje kukufanya uwe kama Adma?+ Nawezaje kukuweka uwe kama Seboiimu?+ Moyo wangu umebadilika ndani yangu;+ na wakati huohuo huruma zangu zimewaka.

  • Luka 15:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Kwa hiyo akaondoka akamwendea baba yake. Alipokuwa angali mbali, baba yake akamwona, akamsikitikia, akakimbia, akamwangukia shingoni na kumbusu kwa wororo.

  • Yakobo 5:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Tazama! Tunawatangaza kuwa wenye furaha wale ambao wamevumilia.+ Mmesikia juu ya uvumilivu wa Ayubu+ nanyi mmeona matokeo ambayo Yehova alileta,+ kwamba Yehova ni mwenye upendo mwororo sana na mwenye rehema.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki