10 Fimbo ya enzi haitageuka kando kutoka kwa Yuda,+ wala fimbo ya kiongozi kutoka katikati ya miguu yake, mpaka Shilo aje;+ na vikundi vya watu vitamtii yeye.+
14 Kwa hiyo Yehova mwenyewe atawapa ninyi ishara: Tazama! Mwanamwali+ kwa kweli atapata mimba,+ naye atazaa mwana,+ naye hakika atamwita jina lake Imanueli.
2 “Nawe, Ee Bethlehemu Efratha,+ wewe uliye mdogo sana kuwa kati ya maelfu ya Yuda,+ kutoka kwako+ atanijia yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli,+ ambaye asili yake ni kutoka nyakati za kale, kutoka siku za wakati usio na kipimo.+
3“Tazama! ninamtuma mjumbe wangu,+ naye atafungua njia mbele zangu.+ Na kwa ghafula Bwana wa kweli+ atakuja kwenye hekalu Lake,+ ambaye ninyi mnamtafuta, na mjumbe+ wa agano+ mnayependezwa naye.+ Tazama! Atakuja hakika,” asema Yehova wa majeshi.+
22 Lakini Sauli akaendelea kupata nguvu hata zaidi naye alikuwa akiwafadhaisha Wayahudi waliokuwa wakikaa Damasko alipokuwa akithibitisha kupatana na akili kwamba huyu ndiye Kristo.+