Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
2 Siku moja baada ya siku nyingine hufanya maneno yabubujike,+
Na usiku mmoja baada ya usiku mwingine huonyesha ujuzi.+
4 Kamba yake ya kupimia imefika duniani pote,+
Na maneno yake yamefika kwenye miisho ya nchi yenye kuzaa.+
Katika hizo amewekea jua hema,+
5 Nalo ni kama bwana-arusi anapotoka katika chumba chake cha ndoa;+
Linashangilia kama mwanamume mwenye nguvu anapokimbia njiani.+
6 Linaenda kutoka mwisho mmoja wa mbingu,
Nao mzunguko wake humalizikia katika ile miisho yake mingine;+
Wala hakuna chochote kilichofichwa kisiweze kupatwa na joto lake.+
7 Sheria+ ya Yehova ni kamilifu,+ huirudisha nafsi.+
Kikumbusho+ cha Yehova ni chenye kutegemeka,+ humfanya asiye na uzoefu awe na hekima.+
9 Kumwogopa+ Yehova ni jambo safi, husimama milele.
Maamuzi ya hukumu+ ya Yehova ni ya kweli;+ yote yameonekana kuwa yenye uadilifu.+