Zaburi
Kwa kiongozi. Wa mtumishi wa Yehova, wa Daudi, aliyemwambia Yehova maneno ya wimbo huu siku ambayo Yehova alikuwa amemkomboa kutoka mkononi mwa adui zake wote na kutoka mkononi mwa Sauli.+ Naye akasema:
18 Nitakupenda wewe, Ee Yehova nguvu zangu.+
2 Yehova ni mwamba wangu na ngome yangu na Mwokoaji wangu.+
Mungu wangu ni mwamba wangu. Nitamkimbilia,+
Ngao yangu na pembe yangu ya wokovu, kilele changu salama.+
4 Kamba za kifo zilinizunguka;+
Mafuriko ya ghafula ya watu wasiofaa kitu pia yaliendelea kuniogopesha.+
6 Katika taabu yangu niliendelea kumwita Yehova,
Nami niliendelea kumlilia Mungu wangu kwa ajili ya msaada.+
Kutoka katika hekalu lake aliisikia sauti yangu,+
Nacho kilio changu cha msaada mbele zake sasa kikafika masikioni mwake.+
7 Na dunia ikaanza kutikisika na kutetemeka,+
Nayo misingi ya milima ikasukasuka,+
Nayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+
8 Moshi ukapanda katika mianzi ya pua yake, nao moto kutoka kinywani mwake ukaendelea kuteketeza;+
Makaa yakawaka moto kutoka kwake.
10 Naye akaja akiwa amepanda juu ya kerubi, akaja akiwa anaruka,+
Naye akaja akiruka juu ya mabawa ya roho.+
Maji yenye giza, mawingu mazito.+
12 Kutoka katika mwangaza ulio mbele yake kulikuwa na mawingu yake yaliyopita,+
Mvua ya mawe na makaa yanayowaka moto.+
13 Na mbinguni Yehova akaanza kunguruma,+
Na Aliye Juu Zaidi akaanza kutoa sauti yake,+
Mvua ya mawe na makaa yanayowaka moto.
15 Na sakafu za vijito vya maji zikaonekana,+
Na misingi ya nchi yenye kuzaa ikafunuliwa,+
Kwa kemeo lako, Ee Yehova, kwa mlipuko wa pumzi ya pua yako.+
17 Alikuwa akinikomboa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+
Na kutoka kwa wale wanaonichukia; kwa sababu walikuwa na nguvu kuliko mimi.+
18 Waliendelea kunikabili katika siku ya msiba wangu,+
Lakini Yehova akawa kama tegemeo kwa ajili yangu.+
19 Naye akanitoa nje mpaka mahali penye nafasi tele;+
Alikuwa akiniokoa, kwa sababu alikuwa amependezwa nami.+
22 Kwa maana maamuzi yake yote ya hukumu yako mbele yangu,+
Nazo sheria zake sitaziondoa kutoka kwangu.+
24 Yehova na anilipe kulingana na uadilifu wangu,+
Kulingana na usafi wa mikono yangu mbele za macho yake.+
25 Kwa mtu mshikamanifu utatenda kwa ushikamanifu;+
Kwa mwanamume asiye na kosa, wewe utatenda kwa njia isiyo na kosa;+
28 Kwa maana wewe mwenyewe utaiwasha taa yangu, Ee Yehova;+
Mungu wangu atafanya giza langu liangaze.+
29 Kwa maana kwa msaada wako ninaweza kukimbiza kikundi cha waporaji;+
Na kwa msaada wa Mungu wangu ninaweza kuupanda ukuta.+
30 Mungu wa kweli, njia yake ni kamilifu;+
Neno la Yehova limetakaswa.+
Yeye ni ngao kwa wale wote wanaomkimbilia.+
32 Mungu wa kweli Ndiye anayenifunga sana mshipi wa nguvu,+
Naye ataifanya njia yangu kuwa kamilifu,+
33 Kuifanya miguu yangu iwe kama ya paa,+
Na kwenye mahali palipo juu kwangu yeye huendelea kunisimamisha.+
35 Nawe utanipa ngao yako ya wokovu,+
Na mkono wako mwenyewe wa kuume utanitegemeza,+
Na unyenyekevu wako mwenyewe utanifanya kuwa mkuu.+
36 Utafanyiza nafasi kubwa ya kutosha kwa ajili ya hatua zangu zilizo chini yangu,+
Navyo vifundo vya miguu yangu hakika havitatetemeka.+
40 Nao adui zangu, utanipa upande wa nyuma wa shingo zao;+
Nao wale wanaonichukia vikali, nitawanyamazisha.+
42 Nami nitawatwanga wawe laini kama mavumbi mbele ya upepo;+
Nitawamwaga kama matope ya barabarani.+
Watu ambao sijawajua—watanitumikia.+
47 Mungu wa kweli ndiye Mpaji wa matendo ya kisasi kwangu;+
Naye hutiisha vikundi vya watu chini yangu.+