1 Petro
Barua ya Kwanza ya Petro
1 Petro, mtume+ wa Yesu Kristo, kwa wakaaji wa muda+ waliotawanyika huku na huku+ katika Ponto, Galatia, Kapadokia,+ Asia, na Bithinia, kwa wale waliochaguliwa+ 2 kulingana na ujuzi wa kimbele wa Mungu Baba,+ kwa kutakaswa kwa roho,+ kusudi wawe watiifu na kunyunyiziwa+ damu ya Yesu Kristo:+
Na mwongezwe fadhili zisizostahiliwa na amani.+
3 Abarikiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo,+ kwa maana kulingana na rehema yake kubwa alituzaa+ sisi upya kwenye tumaini lililo hai+ kupitia ufufuo+ wa Yesu Kristo kutoka kwa wafu, 4 kwenye urithi usioharibika na usiotiwa unajisi na usiofifia.+ Huo umewekwa akiba mbinguni kwa ajili yenu,+ 5 mnaolindwa kwa nguvu za Mungu kupitia imani+ kwa ajili ya wokovu+ ulio tayari kufunuliwa+ katika kipindi cha mwisho cha wakati.+ 6 Nanyi mnashangilia sana katika jambo hilo, ingawa kwa muda kidogo sasa, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa na majaribu ya namna mbalimbali,+ 7 ili sifa iliyojaribiwa ya imani+ yenu, iliyo na thamani kubwa zaidi kuliko dhahabu ambayo huharibika ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto,+ ipatikane kuwa sababu ya sifa na utukufu na heshima wakati wa ufunuo+ wa Yesu Kristo. 8 Ninyi mnampenda,+ ingawa hamkumwona yeye kamwe. Ingawa hammwoni wakati wa sasa, bado mnaonyesha imani katika yeye na mnashangilia sana kwa shangwe isiyosemeka na iliyotukuzwa, 9 huku mkipokea tokeo la mwisho la imani yenu, ule wokovu wa nafsi zenu.+
10 Manabii, waliotoa unabii+ juu ya fadhili zisizostahiliwa zilizokusudiwa ninyi,+ walifanya uchunguzi kwa bidii na kutafuta kwa uangalifu habari kuhusu wokovu huu.+ 11 Waliendelea kuchunguza ni majira gani hasa+ au ni majira ya namna gani ambayo roho+ iliyokuwa ndani yao ilikuwa ikionyesha kumhusu Kristo+ ilipokuwa ikitoa ushahidi kimbele juu ya mateso ya Kristo+ na juu ya utukufu+ ambao ungefuata hayo. 12 Ilifunuliwa kwao kwamba hawakuwa wakijihudumia wenyewe,+ bali walikuwa wakiwahudumia ninyi mambo ambayo sasa mmetangaziwa+ kupitia wale ambao wamewatangazia ninyi habari njema kwa roho takatifu+ iliyotumwa kutoka mbinguni. Malaika wanatamani kuchungulia ndani ya mambo hayo.+
13 Kwa hiyo kazeni akili zenu kwa ajili ya utendaji,+ tunzeni akili zenu kwa ukamili;+ kazeni tumaini lenu juu ya fadhili zisizostahiliwa+ zitakazoletwa kwenu wakati wa ufunuo+ wa Yesu Kristo. 14 Kama watoto watiifu, acheni kufanyizwa+ kulingana na tamaa mlizokuwa nazo hapo zamani katika hali yenu ya kutojua, 15 bali, kwa kupatana na Mtakatifu aliyewaita, ninyi wenyewe pia iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote,+ 16 kwa sababu imeandikwa: “Muwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu.”+
17 Zaidi ya hayo, ikiwa mnamwitia Baba ambaye huhukumu bila ubaguzi+ kulingana na matendo ya kila mmoja, jiendesheni kwa kuogopa+ katika wakati wa kukaa kwenu ugenini.+ 18 Kwa maana mnajua kuwa si kwa vitu vyenye kuharibika,+ kwa fedha au dhahabu, kwamba mlikombolewa+ kutoka kwenye namna ya mwenendo wenu usiozaa matunda ambao ulipokewa kwa njia ya mapokeo kutoka kwa mababu zenu. 19 Bali ilikuwa kwa damu yenye thamani,+ kama ile ya mwana-kondoo asiye na dosari na asiye na doa,+ ile ya Kristo.+ 20 Ni kweli, yeye alijulikana kimbele kabla ya kuwekwa msingi+ wa ulimwengu, lakini alifunuliwa mwishoni mwa nyakati kwa ajili yenu+ 21 ninyi ambao kupitia yeye ni wenye kumwamini Mungu,+ yeye aliyemfufua kutoka kwa wafu+ na kumpa utukufu;+ ili imani na tumaini lenu viwe katika Mungu.+
22 Sasa kwa kuwa mmezitakasa+ nafsi zenu kwa kuwa watiifu kwa ile kweli tokeo likiwa ni upendo wa kindugu usio na unafiki,+ pendaneni sana kutoka moyoni.+ 23 Kwa maana mmezaliwa upya,+ si kupitia mbegu yenye kuharibika,+ bali kupitia ile isiyoharibika+ yenye kuzaa,+ kupitia neno la Mungu+ aliye hai na anayedumu.+ 24 Kwa maana “wanadamu wote ni kama majani,+ na utukufu wao wote ni kama ua la majani; majani hukauka, na ua huanguka,+ 25 bali neno la Yehova linadumu milele.”+ Basi, hili ndilo “neno,”+ hili ambalo ninyi mmetangaziwa+ kuwa habari njema.