Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 9:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Kwa maana mtoto amezaliwa kwetu,+

      Tumepewa mwana

      Na utawala* utakaa juu ya bega lake.+

      Jina lake litakuwa Mshauri wa Ajabu,+ Mungu Mwenye Nguvu,+ Baba wa Milele, Mkuu wa Amani.

       7 Kwa wingi wa utawala wake*

      Na amani, hakutakuwa na mwisho,+

      Kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na juu ya ufalme wake

      Ili kuuimarisha kabisa+ na kuutegemeza

      Kupitia haki+ na uadilifu,+

      Kuanzia sasa mpaka milele.

      Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.

  • Isaya 16:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Kisha kiti cha ufalme kitaimarishwa kabisa katika upendo mshikamanifu.

      Yule anayekikalia katika hema la Daudi atakuwa mwaminifu;+

      Atahukumu kwa haki na kutekeleza uadilifu upesi.”+

  • Yeremia 23:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “Tazameni! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nitakapomwinulia Daudi chipukizi adilifu.*+ Na mfalme atatawala+ na kuwa na ufahamu na kutekeleza haki na uadilifu katika nchi.+

  • Ezekieli 37:24, 25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 “‘“Mtumishi wangu Daudi atakuwa mfalme wao,+ na wote watakuwa na mchungaji mmoja.+ Watatembea katika sheria zangu* na kuzishika amri zangu kwa uangalifu.+ 25 Wataishi katika nchi niliyompa mtumishi wangu, Yakobo, ambamo mababu zenu waliishi,+ nao watakaa humo milele,+ wao na watoto* wao na watoto wa watoto wao;+ na mtumishi wangu Daudi atakuwa kiongozi* wao milele.+

  • Zekaria 12:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Siku hiyo Yehova atakuwa ulinzi kuwazunguka wakaaji wa Yerusalemu;+ siku hiyo yule anayejikwaa* kati yao atakuwa kama Daudi, na nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Yehova anayetangulia mbele yao.+

  • Luka 1:31-33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Tazama! utapata mimba* na kuzaa mwana+ nawe utamwita Yesu.+ 32 Huyo atakuwa mkuu+ naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi,+ na Yehova* Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake,+ 33 naye atatawala akiwa Mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki