Mikutano Ya Utumishi Kwa Januari
Juma Linaloanza Januari 2
Dak 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yanayofaa kutoka kwa Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.
Dak 17: “Mengi ya Kufanya Sikuzote.” Maswali na majibu. Panga kuwe na mahoji mafupi mawili au matatu pamoja na watu wenye shughuli, kama vile mzee, mke wa nyumbani, au painia; waombe waeleze jinsi wameweza kudumisha ratiba kamili na bado wanaendeleza shangwe yao.
Dak 18: “Kutumia Vizuri Vitabu Vyetu vya Zamani.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Julisha kutaniko ni vitabu vipi vya zamani vipatikanavyo; watie moyo wachukue nakala za kutumia shambani. Panga kuwe na onyesho fupi moja au mawili ya utoaji uliodokezwa.
Wimbo 188 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 9
Dak 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Pitia sehemu zenye kupendeza kutoka programu ya “Hofu ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya. Tangaza mipango ya utumishi wa shambani kwa ajili ya mwisho-juma.
Dak 15: “Uchungaji Unaojenga.” Hotuba ikitolewa na mzee inayotegemea habari chini ya kichwa kidogo kwenye kurasa 21-23 za toleo la Mnara wa Mlinzi la September 15, 1993. Kazia shauri la Kimaandiko ili kusaidia kukabiliana na matatizo.
Dak 15: Je! Uko Tayari Kukabili Hali ya Kitiba Yenye Kujaribu Imani? Hotuba yenye uzito lakini yenye kuhamasisha ikitolewa na mzee stadi ili kusaidia akina ndugu wathamini thamani ya ulinzi ya kadi yetu ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia na Kadi ya Utambulishi. Rudia programu ya Januari uliopita ili kuhakikisha kwamba wote wanaostahili na wanaotaka ulinzi huu waweza kuwa nao kwa kujaza kadi hizo. Ona Huduma ya Ufalme Yetu, ya Januari 1994 ukurasa 2, chini ya “Juma Linaloanza Januari 10” kwa maelezo zaidi.
Wimbo 198 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 16
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzia mambo ya kuongea kutoka kwa magazeti ya karibuni. Tia moyo wote washiriki katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Dak 18: “Onyesha Wengine Ufikirio—Sehemu ya 1.” Maswali na majibu. Tia ndani vikumbusha kuhusu uhitaji wa wazee kufanya kazi pamoja kwa ukaribu katika kuangalia kwamba paa, mabomba ya kuleta maji, mifumo ya kiumeme, na maandalizi ya usalama ya Jumba la Ufalme yanarekebishwa vizuri.—Ona Huduma ya Ufalme Yetu ya Desemba 1984, ukurasa 8.
Dak 17: “Onyesha Unajali kwa Kufanya Ziara za Kurudia.” Wahubiri watatu au wanne wazungumza kuhusu kusudi na umuhimu wa kufanya ziara za kurudia. Kazia mradi wa kuanzisha mafunzo. Pitia utoaji uliodokezwa. Panga kuwe na onyesho moja au mawili, na kikundi hicho kikitoa pongezi na madokezo ya uboreshaji.
Wimbo 196 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 23
Dak 5: Matangazo ya kwenu.
Dak 15: Mahitaji ya kwenu, na mahali panapohusika, tia ndani mazungumzo ya eneo lisilohubiriwa kwa ukawaida. Ikiwa kuna wahubiri wanaotaka kusaidia katika eneo la makutaniko ya karibu, mwangalizi wa mzunguko apaswa kujulishwa kupitia Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko.
Dak 10: “Jinsi ya Kupanga Maktaba ya Kitheokrasi.” Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 1994, kurasa 28-31.
Dak 15: “Funzo la Kibinafsi—Jambo la Kuhangaikiwa.” Maswali na majibu. Tia ndani maelezo yaliyoteuliwa yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 1985, kurasa 8-13, (Kiingereza).
Wimbo 116 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 30
Dak 10: Matangazo ya kwenu.
Dak 15: “Kurudi Shuleni Tena.” Kazia matatizo wanayokabili vijana na jinsi wazazi wawezavyo kusaidia watoto wao.
Dak 20: Toa Kitabu Kuishi Milele katika Februari. Elezea ni kwa nini kuna uhitaji wa watu kupata habari ambayo kitabu hiki kinayo. (Ona Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, 1988, kurasa 25-26, mafungu 17, 18.) Simulia kifupi yaliyoonwa yakionyesha uthamini kutoka kwa watu wenye moyo mnyoofu ambao wamekisoma. (Ona Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, 1989, ukurasa 32, na Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, 1991, ukurasa 32.) Toa madokezo fulani kuonyesha jinsi tunavyoweza kuanzisha mafunzo ya Biblia na watu wenye kupendezwa tuliowaangushia kitabu Kuishi Milele. Panga kuwe na mhubiri stadi aonyeshe kifupi utoaji wa pili akitumia chini ya kichwa “Maisha/Furaha” katika kitabu Kutoa Sababu, ukurasa 11, akieleza maana ya msemo “uzima wa milele.” Au tumia utoaji mwingine unaofaa eneo la kwenu. Kumbusha wasikilizaji wachukue fasihi ya kutumia katika utumishi juma hili.
Wimbo 199 na sala ya kumalizia.